Vigogo NIDA waendelea kusota rumande...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
Abdulrahim Sadiki
UPELELEZI
wa kesi ya uhujumu uchumi na kusababisha
hasara ya bilioni 1.16 inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA), Dickson Maimu na wenzake, bado haujakamilika.
Wa kwanza mbele ni Dickson Maimu ambaye aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya vitambulisho (NIDA)
Leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakili
mkuu wa serikali, Vitalis Peter amesema hayo kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius
Mwijage wakati kesi hiyo ilipotajwa.
Peter
amedai upelelezi wa kesi hiyo bado
haujakamilika na kwa upande wa Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Takukuru, Leonard
Swai amedai jalada la kesi hiyo limesharudi kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka
(DPP).
Hakimu
Mwijage ameutaka upande wa Mashtaka ukamilishe upelelezi wa kesi hiyo ili
washtakiwa kama walikula fedha za umma wafungwe au hawajala waachiwe na si kila siku upelelezi
haujakamilika.
Hakimu
Mwijage ameiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 6,2017 na kuutaka upande wa Mashtaka
siku hiyo uje na kitu na siyo upelelezi bado haujakamilika.
Mbali
ya Maimu, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja Biashara wa (NIDA),
Avelin Momburi na Mkurugenzi wa TEHEMA, Joseph Makani.
Kaimu
Mhasibu Mkuu wa NIDA, Benjamin Mwakatumbula, Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste
Insurance Brokers, Astery Ndege, Ofisa
Usafirishaji, George Ntalima, Mkurugenzi
wa Sheria, Sabina Raymond na Xavery Kayombo.
Katika
kesi hiyo, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kutumia madaraka vibaya, kula
njama, kutumia nyaraka za uongo kumdanganya mwajiri na kuisababishia Serikali
hasara ya zaidi ya Sh 1,169,352,931.
Inadaiwa
kwenye shtaka la kwanza Maimu na Mwakatumbula kati ya Januari 15 hadi 19, mwaka 2010 katika makao makuu ya NIDA wilayani Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam,
wakiwa watumishi wa umma kwa nafasi walizokuwa nazo walitumia madaraka vibaya.
Wanadaiwa
kuwa waliidhinisha malipo kwa Gotham International Limited (GIL) ya Dola za
Marekani 2,700,00 bila ya kutumia viwango vya kubadilisha fedha za kigeni
vilivyowekwa na Benki Kuu ya
Tanzania, kinyume na kifungu 19.3 cha
mkataba kati ya NIDA na GIL, hivyo kuifanya GIL kupata faida ya Sh 3,969,000.
Maimu
na Mwakatumbula katika shtaka jingine wanadaiwa kati ya Juni 3 na 5, 2013
katika makao makuu hayo walitumia madaraka vibaya kwa kuidhinisha malipo kwa
GIL ya Dola za Marekani milioni 1.8, bila ya kuzingatia viwango vya kubadilisha
fedha, hivyo kuifanya GIL kupata faida ya Sh 106,346,000.
Washtakiwa
hao wawili wanadaiwa Juni 20, 2014 katika makao makuu hayo, waliidhinisha tena
malipo ya Dola za Marekani 675,000 kwa GIL bila ya kuzingatia viwango vya
kubadilisha fedha, hivyo kuifanya kampuni hiyo kupata faida ya Sh 42,471,000.
Maimu
na Mwakatumbula wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya kwa kupitisha malipo
mengine ya Sh6 milioni kwa GIL bila ya
kupiga hesabu kwa kutumia viwango vya
kubadilishia fedha hivyo kuifanya kampuni hiyo kupata faida ya Sh 14,
661,676.76.
Maimu
na Mwakatumbula wanadaiwa kati ya Januari 15, 2010 na Mei 16, 2015 katika makao
makuu hayo ya NIDA kwa kuidhinisha malipo kwa GIL ya Dola za Marekani bila ya
kuzingatia viwango vya kubadilisha fedha za kigeni waliisababishia NIDA kupata
hasara ya Sh 167,445,676.76.
No comments:
Post a Comment