Wajue mawakili ‘feki’...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Salha Mohamed

WANANCHI wanaohitaji uwakilishi mahakamani wametakiwa kujiridhisha uhalali wa wakili kama amesajiliwa kwa Msajili wa Mahakama Kuu ili kuepuka kutapeliwa na mawakili ‘feki’.

Wakili wa kujitegemea, Leonard Manyama  

Mojawapo ya madhara, ikigundulika wakili hana sifa hata kama umeshinda kesi, hukumu hiyo ufutwa hali ya kuwa ameshamlipa  fedha nyingi

Hayo yamesemwa Dar es Salaam  na mwanasheria ambaye pia ni wakili wa kujitegemea, Leonard Manyama wakati akitoa ufafanuzi wa kisheria wa mtu wa kumuona ili kuwawakilisha mahakamani au kwenye vyombo vya haki kama mawakili wa kujitegemea.

Amesema si kila mwanasheria ni wakili  na anamamlaka ya kuwasimamia watu mahakamani na kwenye mabaraza mbalimbali.

"Mwenye sifa ya kumuwakilisha mtu mahakamani kama wakili wa kujitegemea anapaswa kuwa na sifa tatu, "amesema.

Amesema sifa hizo ni kwa mujibu wa kifungu cha 39 cha sheria ya mawakili sura namba 341.

Amesema moja ya sifa hizo ni jina lake kuwepo kwenye kitabu maalum cha mawakili ambacho kinatunzwa  na msajili wa mahakama kuu.

" Kitabu hicho kinahifadhiwa na msajili wa mahakama Kuu na ndiyo anayo majina yote a mawakili nchini ambao wanauhalali wa kuwawakilisha watu mahakamani, "amesema.

Ameongeza kuwa ili mtu aingie kwenye orodha hiyo anapomaliza masoma ya sheria (law school) anatakiwa kuapishwa na Jaji Mkuu na kupewa cheti cha uwakili.

Amesema sheria inasema mtu huyo anapaswa kuwa  na cheti halali cha uwakili kinachomruhusu kuhudhuria mahakamani.

Amesema sifa nyingine ni kuwa na leseni halali  ya kibiashara  iliyoambatanishwa na nyaraka za maombi ya kupata leseni ya kufanya kazi kama wakili.

" Yeyote ambaye hana vigezo hivi haruhusiwi kwa mujibu wa sheria kumuwakilisha mtu yeyote mahakamani, "amesema.

Amesema kufanya hivyo ni kosa kisheria kwa mujibu wa kifungu cha 41 na 42 cha sheria ya mawakili sura ya 341.

Kinachoeleza kuwa  ni kosa kisheria kwa mtu yeyote ambaye hatambuliki na msajili wa mahakama Kuu kwenda mahakamani kumuwakilisha mtu au kuandaa nayaraka za kisheria.

Amesema endapo wakili akigundulika hana sifa na  hata kama umeshinda kesi, hukumu  hiyo ufutwa hali ya kuwa amelipa fedha nyingi za kuendesha kesi.

Amesema kosa hilo ni la jinai na adhabu yake kifungo cha miezi sita.


"Lakini sheria pia inasema mtu huyo anaweza akapelekwa mahakamani na adhabu yake ni faini isiyopungua na iliyozidi  milioni moja au kufungwa jela miezi 12 au vyote kwa pamoja, "amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search