Hatma ya Mugabe leo, wananchi wapiga kambi Ikulu...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
WAKATI waandamaji nchini Zimbabwe wakiweka kambi nje ya ofisi ya rais Mugabe wakishinikiza ajiuzulu, leo vikao viwili kwa nyakati tofauti vinakutana kujadili hatma ya kiongozi huyo.

Waandamanaji nchini Zimbabwe wakiweka kambi nje ya ofisi ya rais Mugabe kumshinikiza kujiuzulu

Mapema hii leo Mugambe atakutana tena na mkuu wa majeshi, Jen Constantino Chiwenga na baadaye watendaji wakuu wa chama chake cha ZANU-PF

Wapiganiaji wa uhuru ambao hadi kufiki mwaka jana walikuwa watiifu kwa rais Mugabe pia wanasema kwamba rais Mugabe anafaa kung'atuka mamlakani.

Kiongozi wa shirika hilo amewataka raia kuelekea katika makao ya rais Mugabe.

Juzi mara baada ya kikao chake na mkuu huyo wa majeshi, Mugabe alionekana hadharani kwenye mahafali ya moja ya chuo kikuu  mjini Harare Zimbabwe.

Jana waandamanaji nchini humo   walielekea katika afisi ya rais Mugabe ili kumtaka kujiuzulu.

Maandamano hayo yanajiri kufuatia furaha ilioonekana miongoni mwa raia baada ya jeshi kuingilia kati na kumzuia rais Mugabe kwa muda nyumbani kwake siku ya Jumatano.

Wanajeshi katika ikulu ya Whitehouse walioonekana wakiwarudisha nyuma waandamanaji.

Jeshi liliingilia kati baada ya rais Mugabe kumfuta kazi makamu wake wa urais, akionyesha ishara za kutaka mkewe kumrithi.

 Mugabe mwenye umri wa miaka 93 ameiongoza Zimbabwe tangu ilipojipatia uhuru kutoka kwa Uingereza 1980.

Jeshi limehakikisha kuwa anaendelea kukaa katika makoa yake huku likidai kujadiliana naye na kwamba litatangaza kwa wananchi matokeo ya mazungumzo hayo hivi karibuni.



Nje ya ikulu ya rais kuna baadhi ya watu walioketi chini ili kuonyesha pingamizi yao mbele ya majeshi, huku kiongozi wa upinzani, Morgan Tsvangirai akihutubia umati mkubwa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search