Mkuu wa Wilaya: Wanawake acheni kutumia vipodozi vyenye sumu...Soma habari kamili na Matukio360...#share
Na Salha Mohamed
MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amewaasa wanawake kuacha kutumia vipodozi vyenye viambato sumu na watumie vipodozi vya asili ili kujiepusha na saratani.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Mjema ameyasema hayo jijini Dar es Salaam, wakati wa ufunguzi wa kampeni ya Afya na Urembo iliyoandaliwa na Kampuni ya Timeless.
Amesema wapo wanawake wanaotumia vipodozi vyenye viambato sumu ambapo amewataka kupitia mafunzo watakayopata kuwa mabalozi kwa wengine.
"Sasa hivi saratani ni nyingi kwasababu hutujui aidha ni sababu y tunavyokunywa au kupaka, "amesema.
Amesema kupitia kampeni hiyo aliyozindua wanapaswa kuwa mabalozi kwa kutoa elimu ili vipodozi vyenye viambato sumu visiendelee kwani bado watu wanauza.
" Mnajua serikali yetu inakemea vipodozi vyenye viambato sumu, vinavyowaumiza wakinamaa na wakina baba kupitia elimu mtakayotoa itasaidia itasaidia wanawake kutokuwa na rangi mbili, "amesema.
Amesema serikali ipo tayari kuwasaidia kutengeneza bidhaa za asili kwani serikali inapiga marufuku matumizi ya vipodozi ambayo si rafiki kwa mwili wa binadamu.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Timeless, Irene Moshi amesema kampeni hiyo itakuwa endelevu nchi nzima a itatoa ajira kwa vijana.
"kampeni hii itaelimisha na kujifunza kwa pamoja ni namna gani vipodozi vitumike kwao kuwaona kwa watoa huduma, "amesema.
Amesema wapo wanawake waliokuwa na saluni huku akiwa hana utaalamu kupitia kampeni hiyo wamepata na wataweza kutoa huduma nzuri.
Mkuu wa Idara ya huduma za Kinga na Kinywa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Rachel Mhavile wakati akitoa mada ya usafi wa kinywa amesema wanawake hasa wajasiliamali wanapaswa kuwa na kinywa safi.
"Afya y kinywa na meno inamawasiliano na afya ya mwili, harufu mbaya ya kinywa ni fedheha na aibu...madaktari tupo wengi mkapate ushauri, "amesema.
Amesema takwimu zinaonesha watu wengi hupiga mswaki mara moja kwa siku ambapo mtu anatakiwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku na dawa yenye madini ya Floride kwa ulinzi w meno.
MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amewaasa wanawake kuacha kutumia vipodozi vyenye viambato sumu na watumie vipodozi vya asili ili kujiepusha na saratani.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Mjema ameyasema hayo jijini Dar es Salaam, wakati wa ufunguzi wa kampeni ya Afya na Urembo iliyoandaliwa na Kampuni ya Timeless.
Amesema wapo wanawake wanaotumia vipodozi vyenye viambato sumu ambapo amewataka kupitia mafunzo watakayopata kuwa mabalozi kwa wengine.
"Sasa hivi saratani ni nyingi kwasababu hutujui aidha ni sababu y tunavyokunywa au kupaka, "amesema.
Amesema kupitia kampeni hiyo aliyozindua wanapaswa kuwa mabalozi kwa kutoa elimu ili vipodozi vyenye viambato sumu visiendelee kwani bado watu wanauza.
" Mnajua serikali yetu inakemea vipodozi vyenye viambato sumu, vinavyowaumiza wakinamaa na wakina baba kupitia elimu mtakayotoa itasaidia itasaidia wanawake kutokuwa na rangi mbili, "amesema.
Amesema serikali ipo tayari kuwasaidia kutengeneza bidhaa za asili kwani serikali inapiga marufuku matumizi ya vipodozi ambayo si rafiki kwa mwili wa binadamu.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Timeless, Irene Moshi amesema kampeni hiyo itakuwa endelevu nchi nzima a itatoa ajira kwa vijana.
"kampeni hii itaelimisha na kujifunza kwa pamoja ni namna gani vipodozi vitumike kwao kuwaona kwa watoa huduma, "amesema.
Amesema wapo wanawake waliokuwa na saluni huku akiwa hana utaalamu kupitia kampeni hiyo wamepata na wataweza kutoa huduma nzuri.
Mkuu wa Idara ya huduma za Kinga na Kinywa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Rachel Mhavile wakati akitoa mada ya usafi wa kinywa amesema wanawake hasa wajasiliamali wanapaswa kuwa na kinywa safi.
"Afya y kinywa na meno inamawasiliano na afya ya mwili, harufu mbaya ya kinywa ni fedheha na aibu...madaktari tupo wengi mkapate ushauri, "amesema.
Amesema takwimu zinaonesha watu wengi hupiga mswaki mara moja kwa siku ambapo mtu anatakiwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku na dawa yenye madini ya Floride kwa ulinzi w meno.
No comments:
Post a Comment