Babu seya, Papi kocha waachiwa huru, 61 kutonyongwa...soma habari kamili na matukio360...#share

 Na mwandishi wetu
RAIS John Magufuli ametoa msamaha wa kuachiwa huru  kutoka jela kwa familia ya Nguza Vikingi na wafungwa 61 kutonyongwa.

Pia ametoa msamaha kwa wafungwa 8157, kati ya hao 1828 ameagiza kuachiwa huru leo na  waliobaki wamepunguziwe muda wa vifungo vyao.
Rais John Magufuli

Ametoa agizo hilo leo mjini Dodoma katika maadhimisho ya miaka 56 ya uhuru wa Tanzania Bara.

“Nimetoa msamaha wa kuachiwa huru leo hii kwa familia ya nguza Vikingi(Babu Seya) na John Nguza(Papii Kocha). Pia nimetoa msamaha wa kutonyongwa na kuachiwa huru watu 81 waliokuwa miongoni mwa wafungwa waliotakiwa kunyongwa,’’ amesema Magufuli na kuongeza

“Nimewasamehe wafungwa 8157, kati ya hao 1828 waachiwe huru leo, waliobaki nimewapunguzia muda wa vifungo vyao.”

Amesema hatua yake hiyo imezingatia mamlaka aliyopewa na katiba kwa mujibu wa ibara ya 45.

Amesema Tanzania inajumla ya wafungwa takribani 39,000, kati yao wanaume ni 37,000 na wanawake 2000.

 Amesema jumla ya wafungwa 666 wamehukumiwa kifungo cha maisha jela huku wanawake wakiwa ni  11.
“Katika idadi ya waliohukumiwa kunyongwa wanawake ni 19,’’ amesema Magufuli

Amesema kwa mujibu wa idadi ya wafungwa wanaume ni wengi hivyo wajitafakari kwa nini wao ni wengi.

Rais Magufuli amesema mbali na mamlaka aliyopewa kwa mujibu wa katiba, uamuzi wake umezingatia sababu mbalimbali ikiwamo umri, nidhamu na muda waliokaa wafungwa jela.

 “Wapo wafungwa waliohukumiwa kunyongwa wana umri zaidi ya miaka  85, wamekaa zaidi ya miaka 45 jela  na wapo waliotubu makosa yao.

Binadamu wote tunaomba kusamehewa na hata mimi nimeomba kusamehewa na  nimeguswa na hili.  Wengi wao hawakuua albino wala hawakuwa majambazi, hivyo ninatoa msamaha huo,’’ amesema rais

“Yupo aliyefungwa akiwa na miaka 18 na sasa anamiaka zaidi ya 60, huyu anaitwa mzee Maganga Matonya anamiaka 85 amekaa gerezani miaka 37 baada ya kuhukumiwa na alikaa mahabusu miaka 7  ni muhimu nikampa msamaha wa kuachiwa huru,’’


Miongoni mwa magereza yaliyokuwa na wafungwa waliokuwa wamehukumiwa konyongwa na sasa wamepata msahama wa kutonyongwa ni Uyui Tabora wafungwa wawili, Dodoma Isanga  wafungwa 15, Tanga Maweni wafungwa 11, Morogoro Kinguruwila wafungwa 15 na Dar  es Salaam Ukonga wafungwa 19.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search