Magufuli mgeni rasmi uzinduzi ASDP II...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

RAIS John Magufuli anatarajia kuwa mgeni rasim  katika uzinduizi wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) Juni 4, 2018.
Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba amesema programu hiyo inajumuisha wizara za kisekta ambazo ni wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) viwanda, biashara na uwekezaji, wizara ya ardhi, nyumba, maendeleo ya makazi na wizara ya maji na umwagiliaji.

 “Lengo la programu hii ni kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo, mifugo  na uvuvi, kuongeza pato la wakulima wafugaji na wavuvi na kuongeza pato la taifa na kuwa na uhakika wa usalama wa chakula na lishe,” amesema Dk. Tizeba.

Aidha  Dkt Tizeba amesema kuwa ASDP II itatekelezwa katika mikoa na wilaya kwa kuzingatia mazao ya kipaumbele kufuatana na ikolojia ya kilimo ya kanda kwa miaka kumi 10 kwa vipindi viwili vya miaka mitano mitano ambapo kipindi cha kwanza kitaanza 2018/19 hadi 2023/24.

Amebainisha kwamba washiriki wa programu hiyo  ni wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi, ushirika,wizara,Taasisi za serikali na zisizo za serikali, sekta binafsi pamoja na wananchi wote

Katika hatua nyingine waziri Tizeba amekanusha taarifa za kuwa alitengewa bajeti ndogo katika wizara yake katika mwaka wa fedha wa 2018/19 katika bunge la bajeti na kudai bajeti yake iko vizuri na spika wa bunge alikuwa anatania kwani yeye ni mtani wake.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search