Chadema yatoa neno mbunge wake kujiuzulu...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeshangazwa na hatua ya aliyekuwa mbunge wa Siha kupitia chama hicho Dk Godwin Mollel kujiuzulu nafasi hiyo na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kile alichodai ni kwa ajili ya kutetea rasilimali za taifa.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jioni hii kwa umma na Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema John Mrema imesema “Ni jambo la kushangaza kwa kuwa kitendo chake cha kulikimbia Bunge kama chombo cha kusemea na kutetea rasilimali za Taifa na kuja uraiani inatoa taswira gani maana kalikimbia Bunge lenye wajibu huo kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi yetu,” amesema.

“Tunawashauri wale wote ambao wanajitoa waeleze sababu halisi na sio kuhadaa umma kwa sababu uchwara kama hizi, maana wapo wanaosema wanaacha kazi kwenda kuunga mkono dhana ya 'hapa kazi tu' na wengine wanasema wanaenda kuunga mkono juhudi za kuboresha maisha kwa kuacha kazi,” ameongeza.

Amesema Chadema kimepokea taarifa ya kujiuzulu kwa mbunge huyo na kuhamia CCM kupitia mitandao ya kijami.

Mrema ameeleza sababu hiyo aliyotoa ni ya kushangaza kwani Bunge ndicho chombo chenye wajibu wa kusimamia na kulinda rasilimali za Taifa kwa niaba ya wananchi.

Amebainisha kuwa wako imara na wataendelea na ajenda zao bila kuyumbishwa na wimbi hili la watu wachache ambao wameamua kuwasaliti wapiga kura wao kwa kutoa sababu zisizo za msingi ambazo hazina maslahi kwa Taifa bali kwa maslahi yao binafsi . Huu ni ubinafsi wa hali ya juu.

Amesema wataendelea kujenga taifa letu na chama  bila kujali njaa za baadhi yao wala maslahi ya watu wachache na kuongeza kwamba wale wenye dhamira thabiti ndio wataweza kufika mwisho wa safari ya kuleta mabadiliko salama.

Amesema ni dhahiri wale waliotanguliza ubinafsi hawataweza kufika nao mwisho wa safari hii.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search