Ulipaji kodi Zanzibar sasa kwa simu...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Mwajuma Juma, Zanzibar
KAMPUNI ya simu za Mkononi ya Zantel imetiliana saini na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) kwa ajili ya ulipaji wa kodi kwa kutumia njia ya mtandao kupitia huduma ya Easy Pesa.


Utiaji saini huo umefanyika leo  katika ofisi za ZRB Mazizini nje Kidogo ya Mji wa Zanzibar, ambapo kwa upande wa Zantel iliwakilishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo Sheref El-Barbery na ZRB ni Kamishna wa bodi hiyo Amour Hamil Bakir.

Akizungumza mara baada ya utiaji wa saini hiyo Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Amour Hamil Bakir amesema  huduma hiyo inafanyika ili kuwarahisihia wateja wao katika ulipaji wa kodi ambao wamekuwa wakitumia gharama nyingi kufata huduma hiyo ofisini.

Amesema  huduma hiyo imewalenga zaidi wafanyabiashara wadogo.

 Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Sheref El-barbery amesema  ni matarajio yao kwamba huduma hiyo itarahisisha ulipaji  kodi kwa kufanya malipo  ukiwa popote.

Amewataka  wafanyabiashara kutumia  huduma hiyo ambayo itakuwa ni rahisi kwao katika ulipaji wa kodi na kuwapunguzia gharama walizokuwa wakizitumia wakati wa kufata huduma hiyo makao makuu .

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search