Makamu wa rais Samia Suluhu rasmi Dodoma...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu, Dodoma
MAKAMU wa rais, Samia Suluhu kesho  Desemba 15, 2017 anatarajiwa kuamia rasmi mjini Dodoma.

Makamu wa rais, Samia Suluhu

Akizunguma jana alipokuwa akifungua mradi wa nyumba za makazi za Iyumbu Dodoma, rais John Magufuli amesema  kesho Desemba 15, 2017 makamu wa rais ataamia mkoani humo.

Hiyo inamaana shughuli za kiutendaji za kila siku za ofisi za makamu wa rais zitakuwa mjini Dodoma.

‘’Desemba 15, 2017 makamu wa rais atahamia rasmi Dodoma, na mimi rais nitahamia Dodoma mwaka 2018,’’ amesema rais Magufuli
Tayari waziri mkuu, Kassim Majaliwa  ameshahamia mkoani humo na hiyo ni muendelezo wa watumishi wa serikali kuamia mkoani humo.

Tangu alipochukua madaraka ya urais, Magufuli aliahidi serikali yake kuhamia mkoani Dodoma ambako ndiko makao makuu ya nchi kutoka jijini Dar es salaam.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

1 comment

  1. Sawa! Lakini mbona Mugufuli ni mkatili dhidi ya wapinzani wake! Kwa nini wachukia Rais wa Kenya Uhuru Muigai Kenyatta!

    ReplyDelete

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search