Mapinduzi Cup: Simba vs Azam, Yanga na Singida United...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Mwajuma Juma, Zanzibar
KAMATI ya michuano ya kombe la mapinduzi imetangaza ratiba ya michuano hiyo, huku Azam na Simba zikiwa katika kundi moja, Yanga ikiwa na Singida United.



Kikosi cha Yanga

Michuano hiyo itakayotimua vumbi  Desemba 29, 2017, itashirikisha timu 11 huku kundi A  likiwa na timu za Azam, Simba, URA, Jamhuri na Mwenge .

Kundi B kuna timu sita ambazo ni Zimamoto, Mlandege, Taifa ya Jang’ombe, Yanga, JKU na Singida United.

Akizungumza na waandishi wa habari katibu msaidizi wa kamati hiyo, Khamis Shaali amesema  kwa mujibu wa ratiba hiyo siku ya kwanza ya michuano hiyo  mechi tatu  zitachezwa kuanzia majira ya saa 8;00 mchana.  Mchezo wa ufunguzi  ni kati ya Singida United na Mlandege.

Saa 10:00 itafuatia mechi kati ya Zimamoto na Taifa ya Jang’ombe na saa 2:00 usiku Simba atakwaana  uso kwa uso na URA.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search