Ndege ituayo majini yaanza safari...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mashirika ya kimataifa
NDEGE mpya kubwa zaidi
duniani inayoweza kutua na kupaa kutoka majini ya China ya AG600, imefanya safari
yake ya kwanza kwa jumla ya saa moja.
Ndege ya China inayotua majini
Ndege hiyo ambayo ni kubwa
kuweza kukaribiana na ndege ya Boeng ya 747 na yenye injini 4, ilipaa kutoka
uwanja wa ndege wa Zhuhai katika mkoa ulio kusini wa Guangdong.
Ndege hiyo inaweza kubeba watu 50 na kusalia hewani
kwa saa 12. Ina mitambo ya kuzima moto na inaweza kufanya shughuli na uokoaji
baharini na pia inaweza kutumwa kwenda eneo linalozozaniwa kusini mwa habari ya
China.
Vyombo vya habari nchini China viliitaja ndege hiyo
kama mlinzi wa bahari na visiwa. Imechukua miaka minane kuunda ndege hiyo iliyo
na uzito wa tani 53.3.
Kupaa kwa ndege hiyo
kulitangazwa moja kwa moja katika runinga ya taifa na ililakiwa na umati wa
watu waliopeperusha bendera wakati ikitua.
Tayari kuna kandarasi 17 za
kujenga ndege hiyo kutoka ndani ya China. Sera ya China ya kusini mwa bahari
mwa China inapingwa vikali na nchi kadhaa majirani.




No comments:
Post a Comment