Waratibu elimu wawili washushwa vyeo...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu, Kongwa
WARATIBU elimu kata wawili wa kata za Njoge na Lenjulu wilayani Kongwa mkoani Dodoma wameshuswa vyeo kwa makosa ya ulevi na kutokuwajibika katika masuala ya maendeleo mashuleni.
 Mkuu wa wilaya ya Kongwa, Deogratias Ndejembi

Agizo la kushushwa vyeo kwa waratibu hao lilitolewa jana na Mkuu wa wilaya ya Kongwa Deogratias Ndejembi wakati akizungumza na waratibu elimu kata 22 katika kikao cha mapokeo ya kidato cha kwanza na darasa la kwanza mwaka 2018.

Waratibu waliosimamishwa ni Emmanuel Chiluluse wa Kata ya Lenjulu na Venance Mwangasa wa Njoge.

"Hawa watu hawatambui kazi zao hivyo naagiza afisa elimu msingi na sekondari muwatafutie kazi nyingine za kufanya na mtafute watu wengine wa kuziba nafasi zao" alisema Ndejembi.

Ndejembi alisema waratibu wa namna hii hawafai katika wilaya yake kwani wanachochea kushuka kwa kiwango cha elimu na kukiuka ilani ya chama cha mapinduzi (CCM) chini ya mwenyekiti wake Rais John Magufuli,"alisema Ndejembi

Mkuu wa wilaya aliwataka waratibu elimu kata kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wabadirike na kuendana na kasi ya serikaki ya sasa.

Ofisa elimu sekondari wilaya Kongwa Nelson Milanzi alisema waratibu wengi wanajichukulia wao ni waratibu wa shule za msingi na sio sekondari jambo linalofanya msukumo na ufatiliaji wa sekondari kushuka.

Kuhusu ufaulu kwa wanafunzi Milanzi alisema wanafunzi 3863 wamepangwa kuripoti kidato cha kwanza katika shule za sekondari 26 wilayani Kongwa na tayari wakuu wa shule wamepatiwa majina ya wanafunzi hao.

Mwenyekiti wa kamati za kudumu za jamii na diwani wa kata ya Sejeli Chilingo Chimeledya alisema kuna upungufu wa madarasa 20 katika shule zote za sekondari hivyo amewataka viongozi wa kata kushirikiana na wananchi kutatua changamoto hiyo.

Diwani huyo aliwataka viongozi wa kata na wanasiasa kusaidiana na kushirikiana katika kuhamasisha upanuzi wa miundombinu na ujenzi wa madarasa.


Chilingo pia alizungumzia suala la mazingira akiwaomba viongozi wa shule za sekondari Norini, Sagara na Mlali zinazootesha miti kuendelea kugawa katika shule nyingine katika kuboresha mazingira na kutekeleza agizo la makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search