Ni George Weah au Joseph Boakai huko Liberia?...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mashirika ya kimataifa
NCHINI Liberia, leo wananchi wanapiga kura katika duru ya pili ya kumchagua rais wa nchi hiyo kati ya makamu wa rais, Joseph Boakai na nyota wa zamani wa kandanda, George Weah.

George Weah kushoto na Joseph Boakai

Weah mwenye umri wa miaka 51, alishinda duru ya kwanza lakini hakufanikiwa kupata asilimia 50 ya kura kumwezesha kuwa mshindi.

Duru ya pili ya uchaguzi wa urais imechelewa kufanyika  kufuatia kesi iliyokuwa mahakamani.

Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa saa mbili asubuhi na vitafungwa saa kumi na mbili jioni. Zaidi ya watu milioni mbili wamejiandikisha kama wapiga kura.

Boakai mwenye umri wa miaka 73, amekuwa makamu wa rais nchini Liberia kwa miaka 12 lakini haonekani kunufaika na uungwaji mkono kutoka kwa rais Ellen Johnson Sirleaf,.
Naye Weah, ambaye ni nyota wa zamani wa kandanda ana matumaini ya kushinnda baada ya kuwania kwa mara ya tatu.
Alimshinda  Hellen Johnson Sirleaf wakati wa duru ya kwanza mwaka 2005, lakini akashindwa wakati wa duru ya pili kufuatia chama chake kususia duru hiyo ikidai kuwapo kwa udanganyifu.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search