TIA, MUST wachukua ubingwa mashindano vyuo...soma habari kamili na matukio360...#share

Yusta Nkwelengushe,Mbeya

Timu ya Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA) (Wanaume) na timu ya Chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia (MUST)(wanawake) zimefanikiwa kuchukua ubingwa wa michuano ya vyuo yaliyokuwa yakiendelea mkoani hapa .


Timu ya soka ya wanaume ya TIA

Michuano hiyo iliyoshirikisha vyuo nane vilivyopo Mkoa wa Mbeya ilimaliza juzi kwenye Uwanja wa Chuo cha  Teofilo Kisanji University(Teku) ambapo ilishuhudiwa TIA wakiichapa Chuo cha Mtakatifu Agustino (Saut) kwa bao 1-0 ,bao lililofungwa na mshambuliaji Felisian Tonelo dakika ya 19.

Mpambano mwingine ulikuwa ni upande wa Netiboli ambao uliwakutanisha timu ya Must na Saut ambapo Must waliibuka na ushindi wa mabao 17-9 na kufanikiwa kunyakua kombe la Dream Intercollege lililoandaliwa na redio Dream ya jijini hapa.

Katika michuano hiyo zawadi mbalimbali zilitolewa kwa timu  ambapo mshindi wa kwanza alipata Sh300,000 na kombe huku washiriki timu zingine zikipewa vyeti  vya ushiriki wa michuano hiyo mwaka 2017.

Waziri wa Michezo kutoka Saut, Mwegane Yeya alisema walijipanga kuchukua ubingwa wa michuano hiyo lakini dakika 90 ziliamua mshindi na bahati ilikuwa kwa majirani zao TIA.

‘’Ni mwaka wa tatu tunafikia hatua hii ya fainali lakini hatujawahi kuchukua ubingwa ila hatukati tamaa,mwakani tutashiriki tena huenda bahati ikawa upande wetu tukanyakua ubingwa huu,’’alisema Yeya .

Yeya ambaye alinyakua zawadi ya mchezaji mwenye nidhamu alisema mchezo wa soka una matokeo matatu hivyo waliyakubali matokeo hayo.

Naye nahodha wa timu ya TIA, Ibrahimu Daudi alisema  walijipanga kunyakua ubingwa huo na watahakikisha wanajinoa ipasavyo ili mwakani waweze kutetea kombe hilo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search