Vanessa Mdee aibuka kivingine ...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

MSANII wa muziki wa bongo fleva, Vanessa Mdee amezindua albamu yake ya kwanza ya ‘Money Mondays’ yenye nyimbo 18.
Vanessa Mdee na Mohombi Moupondo wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa albamu ' Money Mondays' jijini Dar es Salaam.

Amezindua album hiyo jana jijini Dar es Salaam na nyota wa muziki aliyeshinda tuzo ya kimataifa ya Grammy 2016, Mohombi Moupondo raia wa Sweeden mwanye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia Congo (DRC).

Akizungumza katika uzinduzi huo Vanessa amesema kwenye albamu hiyo ameshirikisha wasanii mbalimbali wa ndani na nje ya nchi na inatarajia kuingia sokoni  Januari  15, 2018.

“Katika albamu hii nimeshirikisha nyota kadhaa wa muziki akiwemo Joh Makini kutoka Tanzania, Caspper Nyovest wa Afrika Kusini, Konshens wa Jamaica na Mahombi,” amesema Vanessa.

Msanii huyo bora wa kike kwa Afrika Mashariki amesema imani yake ni  kwamba albamu hiyo itafanya vizuri kwa kuwafikia watu wengi na lengo ni kuzidi kupenya zaidi katika soko la ndani na nje.

Uzinduzi huo uliohudhuriwa na mastaa mbalimbali ndani na nje ya nchi uliambatana na Vanessa  kuachia nyimbo chache zilizopo katika albamu hiyo ikiwemo ‘Kwangu Njoo’ aliomshirikisha Mohombi.

Vanessa amefanya uzinduzi huo baada ya hivi karibuni kutangaza kusainiwa na lebo ya muziki ya Universal.

Kwa upande wake Mohombi amesema anafurahi kuja kumuunga mkono Vanessa katika uzinduzi huo na kuongeza kuwa ni mategemeo yake albamu hiyo kufanya vizuri kulingana na ubora iliyonayo.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search