WADAU :Ushirikiano unahitajika kudhibiti unyanyasaji....soma habari kamili na matukio360..#share


Na Mwajuma Juma, Zanzibar
WANAHARAKATI wa kutetea haki za wanawake na watoto visiwani Zanzibar wamesema  ushirikiano wa pamoja unahitajika katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia vinavyofanywa kwa wanawake na watoto.
Waziri wa afya Zanzibar , Mahmoud Thabit Kombo

Wakizungumza katika kikao cha kamati cha mradi wa GEWE III kilichokutana ofisi za Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) Zanzibar iliyopo Tunguu mkoa wa Kusini Unguja wamesema hatua iliyofikia ni wazi matendo hayo hayatoweza kuondoka iwapo hakutakuwa na ushirikiano.

Wamesema ushirikiano mdogo  unakwamisha kufuatilia kesi za unyanyasaji.

“Mie nadhani cha msingi ni umoja na ushirikiano tu ndio utakaosaidia kupunguza  vitendo vya unyanyasaji kwa watoto na wanawake. Hii pia itasaidia kufikia malengo tuliyojiwekea”, amesema Sabra Mwinyinjuma Mgeni ambaye ni afisa Wanawake Wilaya ya Magharibi A .

Amesema katika kupambana na kesi hizo ambazo kwa kiasi kikubwa zinaongezeka kila siku ni lazima wajenge ushirikiano kwa kila mmoja kujua kuwa  ni jukumu lake katika kupambana na vitendo hivyo.

“Kila jambo linahitaji umoja, mshikamano na ushirikiano kinyume na hili hatuwezi kufikia kule ambapo tunakokutaka, tujitahidini kuwa na umoja na ushirikiano,” amesema Fatma Juma Jabu ambaye ni Mratibu wa Wanawake wa sehiya ya Mwanakwerekwe wilaya ya Magharibi A Unguja.

Amesema kuna matukio yanatokea lakini   wanashindwa kuyafatilia kutokana kukosa ushirikiano hasa kwa wazee ambao watoto wao wamefanyiwa vitendo vya udhalilishaji.

‘’Pamoja na mambo mengine  umefika wakati kwa wazee kupewa elimu zaidi ili wanapopata tatizo waripoti na baadae watoe ushirikiano na wasiogope kuona kuwa mambo yao yatakuwa wazi.’’





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search