Takukuru yamkamata mgombea wa CCM...soma habari kamili na matukio360..#share


Na mwandishi wetu, Singida
TAASISI ya kupambana na kudhibiti rushwa(TAKUKURU) inamshikilia mshindi wa kura za maoni CCM jimbo la Singida Kaskazini (kabla ya kufutwa), Haider Gulamali kwa tuhuma za kutoa rushwa.

Haider Gulamali 

Hatua hiyo inafuatia baada ya jana CCM kufuta mchakato wa kura ya maoni uliofanyika katika jimbo la Singida kaskazini kutokana na baadhi ya wagombea kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Katibu wa Nec-Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alisema kutokana na hali hiyo  Haider Gulamali na Elia Mlangi wamezuiwa kugombea nafasi hiyo kutokana na kutuhumiwa kujihusisha na rushwa.

CCM imewataka wote wenye nia ya kutaka kuteuliwa na chama hicho  kugombea ubunge wachukue fomu kesho Alhamisi  na wazirudishe jioni ya siku hiyo. Awali jumla ya wagombea 17 walijitokeza kuwania nafasi hiyo.

Tayari tume ya uchaguzi imetangaza uchaguzi wa jimbo hilo na mengine mawili kufanyika Januari 13, 2018. Kata sita nazo zitashiriki katika uchaguzi huo wa marudio. Majimbo mengine ni Longido Kaskazini na Songea mjini.

Haider Gulamali ambaye ni mfanyabiashara mwenye asili ya Kiasia mjini Dodoma, aliibuka wa kwanza kwenye kura za maoni kugombea nafasi ya ubunge kwa tiketi ya CCM jimbo la Singida Kaskazini kwa kupata asilimia 60.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search