Watoto 52 wazaliwa mkesha Krismass... soma habari kamili na matukio360..#share
Na Salha Mohamed,Dar es salaam
JUMLA ya watoto 52 wamezaliwa mkesha wa Krismass katika hospitali ya taifa ya rufaa Muhimbili (MNH), Amana na Temeke.
Mwanahamisi Omar mkazi wa Mbagala akiwaangalia watoto wake mapacha aliojifungua usiku wa kuamkia chrismass,Mwanahamisi alipata rufaa kutoka hospitali ya Zakhem
Akizungumza Dar es Salaam leo na matukio360, Muuguzi Mwandamizi MNH, mariam Mlawa amesema wanawake sita wamejifungua katika hospitali hiyo.
Amesema wanawake wawili walijifungua watoto mapacha ambapo mmoja alijifungua kwa upasuaji.
"Wazazi sita walijifungua usiku wa kuamkia leo, wazazi wawili walijifungua kwa upasuaji na wanne walijifungua kawaida, mzazi mmoja alijifungua mapacha kwa upasuaji,"amesema.
Amesema hakuna tofauti kwa uzazi wa mwaka huu na mwaka jana na kuongeza kuwa wazazi watano walipata rufaa kutoka hospitali zingine huku mmoja akitumia bima ya afya.
"Afya za mama pamoja na watoto hao zinaendelea vizuri,"amesema.
Katika hatua nyingine,Ofisa Muuguzi Kiongozi hospitali ya Temeke,Rashid Ally amesema katika mkesha wa krismass wamezaliwa watoto 12 ambapo wakike ni watatu na wakiume wakiwa tisa.
"Hakuna upasuaji wala waliojifungua mapacha na Afya zao zinaendelea vizuri, "amesema.
Aidha, Muuguzi wa zamu hospitali ya Amana, Agnes Simon amesema waliojifungua ni 32 ambapo watoto wakiume ni 18 na wakike 14 huku wazazi watano walijifungua kwa upasuaji.
JUMLA ya watoto 52 wamezaliwa mkesha wa Krismass katika hospitali ya taifa ya rufaa Muhimbili (MNH), Amana na Temeke.
Akizungumza Dar es Salaam leo na matukio360, Muuguzi Mwandamizi MNH, mariam Mlawa amesema wanawake sita wamejifungua katika hospitali hiyo.
Amesema wanawake wawili walijifungua watoto mapacha ambapo mmoja alijifungua kwa upasuaji.
"Wazazi sita walijifungua usiku wa kuamkia leo, wazazi wawili walijifungua kwa upasuaji na wanne walijifungua kawaida, mzazi mmoja alijifungua mapacha kwa upasuaji,"amesema.
Amesema hakuna tofauti kwa uzazi wa mwaka huu na mwaka jana na kuongeza kuwa wazazi watano walipata rufaa kutoka hospitali zingine huku mmoja akitumia bima ya afya.
"Afya za mama pamoja na watoto hao zinaendelea vizuri,"amesema.
Katika hatua nyingine,Ofisa Muuguzi Kiongozi hospitali ya Temeke,Rashid Ally amesema katika mkesha wa krismass wamezaliwa watoto 12 ambapo wakike ni watatu na wakiume wakiwa tisa.
"Hakuna upasuaji wala waliojifungua mapacha na Afya zao zinaendelea vizuri, "amesema.
Aidha, Muuguzi wa zamu hospitali ya Amana, Agnes Simon amesema waliojifungua ni 32 ambapo watoto wakiume ni 18 na wakike 14 huku wazazi watano walijifungua kwa upasuaji.
No comments:
Post a Comment