Baraza la vyama vya siasa wachaguana....soma habari kamili na matukio 360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

BARAZA la vyama vya siasa nchini limefanya uchaguzi wa viongozi wa kamati nne huku kila kamati ikiwa na mwenyekiti na makamu mwenyekiti ambao wataongoza kamati hizo kwa muda wa miaka miwili kwa mujibu wa sheria.

Pia limetoa siku 30 kwa kamati ya sheria na utawala bora ya baraza hilo kuhakikisha inajadili mapendekezo ya sheria na kanuni mpya ya vyama vya saisa kisha kuleta mrejesho.

Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa na Mwenyekiti wa TADEA John Shibuda akizungumza katika mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika kwenye ukumbi wa Mkwawa ofisi Ndogo za Bunge jijini Dar es salaam kulia Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Bw. Sisty Nyahoza.

Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa baraza hilo John Shibuda akizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao cha baraza hilo kilichokuwa kimeketi jijini Dar es Salaam

Miongoni mwa viongozi waliochaguliwa ni John Momose Cheyo kutoka chama cha UDP ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya fedha na Salum Mwalimu kutoka chama cha Chadema ambaye ni Makamu Mwenyekiti.

Kamati ya bunge na siasa, mwenyekiti ni Juju Martin Danda kutoka chama cha NCCR-Mageuzi na makamu mwenyekiti ni Mohamed Masoud Rashid kutoka chama cha Chauma.

Kamati ya sheria na utawala bora itaongozwa na mwenyekiti Hassan K. Almas kutoka chama cha NRA na Said Soud kutoka chama cha AFP ambaye ni  Makamu Mwenyekiti.

Kamati ya Maadili na Mahusiano ni  Mohammed Ali Abdullah kutoka chama cha Demokrasia Makini ambaye ni Mwenyekiti na Peter A. Magwira kutoka chama cha DP ndiye Makamu Mwenyekiti.

Viongozi wa kamati za baraza wamechaguliwa kwa kupigiwa kura ya siri na wajumbe wa kila kamati. Mwenyekiti akitokea upande mmoja wa Tanzania, Makamu Mwenyekiti atatokea Zanzibar.

Wenyeviti wa kamati za Baraza la vyama vya siasa, Mwenyetikiti wa Baraza la vyama vya siasa na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la vyama vya siasa ndio huunda kamati ya Uongozi ya vyama vya siasa.


Kuhusu siku 30, Shibuda amesema “Barazala vyama vya siasa nchini limeazimia kwa kauli moja kuwa mjadala wa mapendekezo ya Sheria na Kanuni mpya ya vyama vya siasa, utaanzia kwenye kamati ya Sheria na utawala bora”, amesema.

Ameongeza “Itajadili mapendekezo tata yaliyokusanywa kutoka kwa wadau mbalimbali  na pia kamati itakuwa na jukumu la kukusanya upya maoni ya mapendekezo ya kutunga sheria na kanuni mpya ya vyama vya siasa, tumeipa siku 30 kukamilisha kazi hiyo, lakini ikitaka tuiongeze muda tutafanya hivyo,”.

Shibuda amesema kamati hiyo ikikamilisha kazi yake italeta mrejesho mbele ya  baraza kwa maboresho na wajumbe wakiridhia yatawasilishwa kwenye mamlaka husika kwa ajili ya kukamilisha utaratibu wa utungaji wa Sheria na Kanuni mpya ya vyama vya siasa.

Amesisitiza kuwa kwa sasa sheria na kanuni za vyama vya siasa zilizopo zitaendelea kutumika hadi hapo zitakapotungwa sheria mpya.
 


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search