Chadema wavunja makubaliano ya Ukawa...soma habari kamili na matukio 360...#share
Na mwandishi wetu,Dar es salaam
CHAMA cha Chadema kimebadilisha msimamo wake na sasa kinashiriki uchaguzi wa marudio wa Ubunge katika jimbo la Kinondoni na Siha utakaofanyika Februari 17,2018
Mwaka jana kwa niaba ya Ukawa, mwenyekiti taifa wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza kutoshiriki uchaguzi wowote mdogo wa marudio hadi hapo NEC itakapokutana na wadau wa vyama vya siasa kujadili na kuondoa kero na vikwazo vilivyojitokeza katika uchaguzi wa udiwani wa kata 43 wa mwezi Novemba,2017
CHAMA cha Chadema kimebadilisha msimamo wake na sasa kinashiriki uchaguzi wa marudio wa Ubunge katika jimbo la Kinondoni na Siha utakaofanyika Februari 17,2018
Mwaka jana kwa niaba ya Ukawa, mwenyekiti taifa wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza kutoshiriki uchaguzi wowote mdogo wa marudio hadi hapo NEC itakapokutana na wadau wa vyama vya siasa kujadili na kuondoa kero na vikwazo vilivyojitokeza katika uchaguzi wa udiwani wa kata 43 wa mwezi Novemba,2017
TAARIFA KWA UMMA,
KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA KINONDONI NA SIHA.
Kamati Kuu ya
Chama imemaliza Vikao vyake Leo tarehe 19 Januari, 2018 na imefanya uamuzi wa
kushiriki kwenye uchaguzi mdogo kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha
unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 Februari, 2018.
Baada ya uamuzi
huu kufanyika , Kamati Kuu imewateua wagombea wa Majimbo hayo kama ifuatavyo;
1. Jimbo la Kinondoni ameteuliwa Mhe. Salum
Mwalim Juma.
2. Jimbo la Siha ameteuliwa Bwana Elvis
Christopher Mosi.
Wagombea wote
wameshachukua fomu za uteuzi kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo
husika na watazirejesha kesho Jumamosi tarehe 20 Januari 2018 , kwa ajili ya
uteuzi.
Imetolewa Leo
tarehe 19 Januari, 2018.
John Mrema -
Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje
No comments:
Post a Comment