IGP Sirro amkabili 'nabii' anayeendesha ibada katika baa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MKUU wa jeshi la polisi, IGP Simon Sirro amefanya mazungumzo na Tito Machija anayejihita nabii ambaye amekuwa akionekana mitandaoni akifanya mambo yasiyoendana na maadili ya dini na injili anayodai kuihubiri katika baa.

Hata hivyo inadaiwa baada ya mazungumzo hayo jeshi la polisi mkoani humo lilimkamata kwa mahojiano zaidi

IGP Sirro akizungumza na Nabii Tito mjini Dodoma leo.

IGP Sirro  amezungumza na ‘mhubiri binafsi’ huyo licha ya jeshi hilo kutotoa taarifa rasmi ya kilichojiri na utaratibu unaoendelea iwapo ni kumhoji au kumfikisha mahakamani.

Nabii huyo ambaye video zake zimekuwa zikisambaa zikihamasisha kuoa mke zaidi ya mmoja, kufanya ngono na wafanyakazi wa ndani,  anatumia pombe kupata waumini na anadai hataki nyimbo za injili kwenye ‘ibada’ zake, na  baadhi at ibada zake hufanyia baa.


Pia ameonekana akicheza nyimbo za bongo fleva akiwa  ‘madhabahuni’ badala ya kwaya na huku akieleza kuwa wafadhili wake wanatumia pombe,  hivyo na yeye lazima waumini wake watumie pombe ambazo amezifanyia upako.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search