Jaji mkuu: Tutawahoji, kuwachukulia hatua wote wanaoingilia uhuru wa mahakama....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es salaam

MAHAKAMA nchini imesema inatarajia kuunda kamati ya maadili kama ya Bunge itakayokuwa na uwezo wa kuchukua hatua stahiki kwa wote watakaoingilia uhuru wa mhimili huo wa nchi
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Juma akizungumza jijini Dar es Salaam kuhusu maonesho ya wiki ya sheria itakayoaanza Januari 27 hadi Januari 30, 2018.

Pia imesema majaji na mahakimu ndiyo wenye wajibu na jukumu la kuhakikisha wanalinda uhuru wa mhimili huo na kwamba wanatakiwa kuwaita wanaouingilia, kuwahoji na kuwachukulia hatua inapobidi.

Msimamo huo umetolewa leo jijini Dar es salaam na Jaji mkuu, Profesa Ibrahimu Juma alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya maadhimisho ya wiki ya sheria nchini yanayotarajia kufanyika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.

“Inatakiwa ifike mahali kufanya kama Bunge, kuunda kamati ya maadili itikayo wawajibisha wanaoingilia muhimili huu, mfano mtu anapolikosea Bunge anaitwa kwenye kamati na kuhojiwa, lakini niwatake Mahakimu na Majaji wasiruhusu mtu yeyote kuingilia uhuru wa mahakama,” amesema jaji mkuu  Prof. Juma.

Amesema sababu ya mihimili kuingiliana ni kutokana na kutokufuatwa kwa kanuni, taratibu na katiba ya nchi na kuwa ili kuondoa hali hiyo kila mhimili unatakiwa kufuata mamlaka iliyopewa  .

“Ninawakumbusha wananchi na viongozi mbali mbali nje ya mahakama kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania mamlaka ya utoaji haki ni ya mahakama tu, na nawasihi viongozi wote wa serikali wenye mamlaka ya kikatiba na kisheria wabaki ndani maeneneo yao ya kikatiba na wajiepushe kuingilia maneo yaliyo ndani ya haki, hadhi na mamlaka kikatiba ya maahakama,” amesema 

Akizungumzia kuhusu wiki ya sheria, amesema siku ya sheria itakuwa Februari 1, 2018 na ni siku maalum ambayo itaashira kuanza kwa shughuli za mahakama kwa mwaka huu.

Hivyo kabla ya siku hiyo mahakama pamoja na wadau muhimu katika sekta ya sheria watatumia siku tano kuanzia Januari 27 hadi Januari 30, 2018 kutoa elimu ya sheria kwa wananchi watakaopata nafasi ya kuhudhuria na hiyo itakuwa sehemu ya maadhimisho ya siku ya sheria.

Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma amesema kilele cha maadhimisho hayo itakuwa Februari 1, 2018 katika viwanja vya mahakama vilivyopo mtaa wa Chimala jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais John Magufuli.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search