Kocha mpya Simba asema miezi miwili tu mtaona mambo yangu...soma habari kamili na matukio 360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

KLABU ya Simba leo imemtambulisha kocha mpya Mfaransa Pierre Lechantre na wa viungo Mtunisia Aymen Habib. Kocha huyo amesema kikosi chake kitaeleweka baada ya miezi miwili.
Kocha mpya wa Simba Pierre Lechantre (katikati) akiwa ameshika  jezzi ya simba (wakwanza kushoto) ni kaimu rais wa Simba, Salim Abdallah na wa mwisho kulia ni Meneja wa kocha huyo Joe Onegofro  jijini Dar es salaam.

Akizungumza baada ya kusaini  makubaliano ambayo hayakuwekwa wazi, kocha hiyo amesema atakuwepo kwa muda mrefu kwa kuwa klabu ina malengo ya muda mrefu kwa ajili ya kuwa bora barani Afrika.

“Nipo hapa kwa ajili ya ‘project’ ya muda mrefu ili kuhakikisha timu inakuwa bora, ninaweza kuwepo hapa kwa miaka mitatu au zaidi,” amesema Lechantre.

Amewetaka kwa sasa mashabiki na wapenzi wa mpira nchini kuweka pembeni wasifu wake na waangalie kazi ambayo amekuja kuifanya na kueleza kuwa mabadiliko katika timu yanaweza kuanza kuonekana baada ya miezi miwili.

Kwa upande wake msemaji wa Simba Haji Manara, amesema kocha huyo atasaidia pia katika maendeleo ya timu za vijana kwani klabu inamalengo makubwa.

Pia amewataka mashabiki wasimba kuwa na uvumilivu pale klabu inapofanya vibaya kwani hakuna anayependa kutokea jambo hilo.

Kocha mpya wa simba Pierre Lechantre akibadilishana mkataba na kaimu rais wa simba Salim Abdallah baada ya kutiliana saini jijini Dar es Salaam.



Kaimu rais wa Simba Salim Abdallah akiwa ameshika jezi yenye jina la kocha wa viungo Aymen Habib.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search