Polisi watoa onyo waliotoka kwa msamaha wa rais...soma habari kamili na matukio360....#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
JESHI la Polisi Kanda
Maalum ya Dar es Salaam limeto onyo kali kwa waliotoka gerezani kwa msamaha wa
rais ambao hawataki kubadilika kitabia na kifikra ili kuishi kwa mujibu wa
sheria za nchi.
Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam SACP Lazaro Mambosasa, akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa.
Onyo hilo limetolewa leo jijini hapa na
Kamanda wa Polisi kanda hiyo SACP Lazaro Mambosasa akizungumza na waandishi wa
habari, amesema hatua hiyo inakuja baada kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili wakiwa na silaha aina ya AK 47 yenye namba UC
49331998 ambayo haikuwa na magazine yake.
Watuhumiwa
waliokamatwa ni Ally Makwaya (40) mkazi wa Tandale kwa Tumbo na Fredrick
Odhiambo (50) mkazi wa Tandale kwa Tumbo.
Katika mahojiano kuhusu wapi waliipata silaha hiyo walieleza kuwa shughuli zao kubwa ni kuokota makopo na vyuma chakavu na kuwa hata silaha hiyo waliiokota huko eneo la karakana (garage) Kinondoni Mwinyijuma.
Katika mahojiano kuhusu wapi waliipata silaha hiyo walieleza kuwa shughuli zao kubwa ni kuokota makopo na vyuma chakavu na kuwa hata silaha hiyo waliiokota huko eneo la karakana (garage) Kinondoni Mwinyijuma.
“Natoa onyo kali kwa
mtu yeyote ambaye amepata msamaha badala ya kumshukuru Mungu akabadili tabia,
kubadilika kifikra, akaanza kuishi kwa kufuata sheria za nchi, anarudi kwenda
kufukua silaha mahali alipoificha kwa ajili ya kuendeleza vitendo vya kihalifu
niwaambie hawatabaki salama tutawakamata na tutawarudisha huko walikotoka,” amesema SACP
Mambosasa.
“Taarifa tulizonazo
baadhi ya wahalifu wachache walioachiwa kwa msamaha wa rais ambao hawataki
kubadili tabia zao wamekwenda sasa kufichua silaha ambazo walizizika ardhini na
wanaziibua kwa ajili ya kuanza kuzitumia,” ameongeza.
Ameeleza, wengine
wanashirikiana na wenzao ambao bado wako jela kwa kuwatuma mahali walipozificha
silaha na kuingia nazo mtaani.
Amesema kuwa mtu akipata
msamaha kitu cha kwanza anachotakiwa kufanya ni kumshukuru Mungu na kubadilika
ili kufanya matendo ambayo hayavunji sheria za nchi.
Kwa mwingine
jeshi hilo linawashikilia watu nane kwa makosa mbali mbali ya uhalifu.
SACP Mambosasa
amesema miongoni mwa watuhumiwa hao wawili walikamatwa Januari 3, 2018 majira
ya 03:30 maeneo ya Sinza karibu na kituo cha kuuza mafuta cha Big Bon na
waliokamatwa ni Abdulkareem Bashir (24) na Emmanuel John Bundala (22)
mwanafunzi wa Veta mwaka wa tatu kwa kujihusisha na matukio ya wizi wa
magari,vifaa vya magari na wizi katika benki kwa kutumia “Master Cards na
Master Keys”.
Katika tukio
lingine, amesema watuhumiwa sita
walikamatwa wakiwa na vielelezo mbalimbali, television nane (8), Subwoofer 1 ya
Samsung na spika nne vilivyokuwa vimefichwa nyumbani kwa mtuhumiwa mmojawapo.
No comments:
Post a Comment