ACT wamtaka msemaji wa serikali kuacha 'propaganda'....soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
CHAMA cha ACT-Wazalendo
kimemtaka Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hassan Abasi kuacha propaganda kwa kile
walichodai kwamba anafanya upotoshaji kuwa nchi inafanya vizuri kwenye uchumi,
demokrasia, utawala bora na haki za kiraia.
Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Msimamizi huo imetolewa
leo jijini Dar es Salaam na Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu alipokuwa akitoa
taarifa ya ziara za viongozi katika maeneo mbali mbali nchini pamoja na
mafanikio ya chama kwa miezi miwili ya Januari na Februali 2018.
“Hizi ni kauli za
kejeli, huwezi ukasema kwa mfano Tanzania imeimarika katika utawala bora, kila
mmoja anafahamu leo ni mwathirika mara dufu katika utawala wa awamu ya tano
kwenye suala la haki za kiraia, haki za binadamu na utawala bora na demokrasia,”
amesema Shaibu.
Amedai msemaji
huyo amekuwa akinukuu takwimu mbali mbali za ndani na nje nchi kuhalalisha hoja
zake ambazo kama ACT-Wazalendo wameona kuwa ni propaganda.
Shaibu amesema amekuwa akitoa taarifa za ripoti bila kuzisoma kwa undani na kuelezea kwa
uhalisia kilichoandikwa kuhusu hali ya nchi kwa mwaka huu na ilivyokuwa kwa
miaka iliyopita.
“Kwa mfano ukisoma
ripoti ya democracy Index inaonesha kwamba ukilinganisha mwaka 2017 na 2016 ni
tofauti tumeshuka, 2016 ripoti inaonesha tulipata alama 5.76 wakati 2017
tumepata alama 5.47 huko ni kushuka, msemaji hawezi kusema haya,” ameongeza.
Ameongeza kuwa kwa
mujibu wa ripoti hiyo ya mwaka jana 2017 inaonyesha Tanzania kudondoka zaidi
kwenye eneo la haki za kiraia kutoka alama 5 kwa mwaka 2016 hadi alama 4.7
mwaka 2017.
Amebeinisha kwamba
kumekuwepo kwa kushuka kwenye eneo la utawala bora, demokrasia na haki za
binadamu ambapo amesema ripoti ya uwazi katika bujeti (Open Budget Index
inayotolewa na Taasisi ya International Budget Partnership (IBP) inaonesha
Tanzania imeporomoka kwa kasi kwenye eneo la uwazi kwenye bajeti kwa kupata
alama 10 mwaka 2017 ukilinganisha na alama 46 za mwaka 2016.
Amemtaka msemaji wa
serikali aache tabia ya kuchukua taarifa vipande vipande na kuziweka kwa umma.
Akizungumzia kuhusu
ziara za viongozi wao, Shaibu amesema kuwa Februari 14, 2018 hadi Februari 25,
2018 Mwenyekiti wa chama Yeremia Maganja atafanya ziara kwenye mikoa ya Lindi,
Mtwara, Pwani, Tanga, Arusha na Kilimanjaro. Ataambatana na Mohammed Massanga,
Katibu wa kapeni na chaguzi.
Amesema Makamu
mwenyekiti Shaaban Mambo akiambatana na naibu katibu mkuu Bara Msafiri Mtemelwa
na Katibu wa Itikadi na Uenezi Ado Shaibu watafanya ziara kwenye mikoa ya
Dodoma, Singida, Geita, Simiyu na Kagera kuanzia Februari 14, 2018 hadi
Februari 23, 2018.
Katika mafanikio
amesema kwa mwaka huu wamejiwekea vipaumbele vinne ambavyo ni kuimarisha muundo
wa chama kupitia chaguzi, kuimarisha ushirikiano na vyama ya wafanyakazi,
kuimarisha ushirikiano na vyama vingine vya siasa na kuendelea kushawishi sera
za uchumi zinazomkomboa mwananchi.
Kwenye vipaumbele hivyo
wamefanikiwa mambo mawili kupitia mwakilishi wao bungeni Zitto Kabwe kwa
kushirikiana na wabunge wenzake. Mambo hayo kuondolewa kwa kodi kwenye mafao ya
wastaafu na Fao la matibabu kwa wanachama wa NSSF.
No comments:
Post a Comment