ANC yaadhimisha miaka 100 kuzaliwa Nelson Mandela.....soma habari kamili na matukio360.....#share

Na mashirika ya kimataifa
Chama tawala cha Africa Kusini ANC kimeanza maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka mia moja tangu kuzaliwa kwa rais wa kwanza mweusi nchini humo shujaa, Nelson Mandela.
hayati Nelson Mandela
Kiongozi wa sasa wa ANC ,Cyril Ramaphosa anatarajiwa kutoa hotuba huko medani mwa Freedom square mjini Cape Town, ambako marehemu Mandela alitoa hotuba yake ya kwanza alipoachilia huru kutoka gerezani miaka ishirini na nane iliyopita.
Rais Jacob Zuma ambae anakabiliwa na madai chungu nzima ya rushwa amegoma kubanduka huku shinikizo za kumtaka ajiuzulu zikizidi kumzonga .
ANC imetangaza mkutano maalum wa kamati yake kuu ya kitaifa utafanyika Jumatatu kujadili swala hilo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search