Kikosi cha Simba dhidi ya Gendamarie Tnale hiki hapa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

KOCHA Mkuu wa klabu ya Simba SC,  Pierre Lechantre ametangaza kikosi ambacho kinaivaa jioni hii klabu ya Gendamarie Tnale kutoka Djibouti kwenye mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Katika mchezo huu Simba wanaingia wakiwa kama wenyeji ambao utachezwa kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Simba itaongozwa katika safu ya ushambuliaji na wachezaji wake muhimu John Bocco na Emmanuel Okwi wakitumia mfumo wao wa 3-5-2.
Kikosi kamili cha Simba SC kinachowavaa Gendarmerie.
Mchezo utachezwa majira ya saa 10:00 jioni na utaonesha mubashara na kituo cha Runinga cha Azam TWO.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search