CCM waituhumu Chadema.....soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam
CHAMA cha CCM kimedai kuhujumiwa na chama cha Chadema kwa vijana wake kutekwa, kupigwa, kuumizwa na wanachadema
Pia kimetuhumu kuwa Chadema kimeleta watu kutoka mikoani ili kuharibu uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Kinondoni.
Pia kimetuhumu kuwa Chadema kimeleta watu kutoka mikoani ili kuharibu uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Kinondoni.
Katibu wa Itikazi na Uenezi wa Chama cha Panduzi (CCM) Humphrey Polepole akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Katibu wa Itikadi
na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa uchaguzi mdogo
wa marudio ya ubunge katika majimbo ya Siha, Kinondoni na udiwani katika kata
10.
“Tunazo taarifa za Chadema kuwaleta watu kutoka mikoani kwa kigezo
cha kulinda kura, zipo nyumba kadhaa zimewahifadhi, tumeshatoa taarifa kwa
jeshi la polisi juu ya watu hawa, hivyo ni kazi ya polisi kufuatilia na
kuchukua hatua,” amesema Polepole.
Polepole amesema kura hazilindwi na kila mtu bali kuna
utaratibu uliowekwa na Tume ya Uchaguzi nchini (NEC) ya namna ya kuzilinda na
wahusika ni mawakala wa vyama walioteuliwa kuwakilisha.
Akizungumzia kuhusu hujuma za Chadema dhidi yao, amedai kuwa
Mwananyamala kuna kijana wa CCM alipigwa na kuchomwa bisibisi mgongoni.
Pamoja na kutoa taarifa polisi amedai kuwa wanachadema
hawakukoma, waliwateka na kuwaficha vijana wa kike wa CCM ndipo kwa
kushirikiana na jeshi la polisi waliwafuatilia na kuwakamata.
Akizungumzia kuhusu
uchaguzi wa katika jimbo la Siha na kinondoni amejinasibu CCM
itashinda kwa kishindo na kwa zaidi ya asilimia 50.
Amesema uhakika huo ni kutokana na kwamba chama hicho kina
mtaji wa wanachama milioni 12 nchi nzima kati ya wapiga kura milioni 25 hivyo
kutokana na takwimu hizo wanauhakika kushinda pasipo hata kupiga kampeni.
Amedai kinachosubiriwa ni kuwapongeza washindi na
kufanya sherehe na kwamba hiyo ni ishara kwamba chama kitashinda pia kwa
kishindo katika uchaguzi mkuu wa 2020.
Ameliomba jeshi la polisi kuhakikisha kunakuwepo na usalama,
amani na utulivu siku ya uchaguzi ili wananchi wajitokezi na kutimiza haki yao
ya kikatiba ya kuchagua viongozi wao.
Katika hatua nyingine Polepole amesema yupo mbunge mmoja wa Chadema jijini Dar es Salaam ambaye mara kadhaa amekuwa akiomba kujiunga na CCM lakini wamemkatalia.
“Yupo kiongozi mmoja hapa Dar es Salaam wa Chadema, ameomba
sana tumemkataa ni gunia la michongoma, tumemkataa yeye anajua,” ameeleza.
Amedai kiongozi huyo hajafanya lolote la kimaendeleo katika
jimbo lake hadi sasa na kwamba ameshamwambia 2020 atafute kazi nyingine ya
kufanya kwani hatashinda.
Pia Polepole amedai wapo wabunge wanne na madiwani wa jijini Dar es salaam kutoka vyama vya upinzani ambao wanasubiri kuwapokea
Amesema sababu ya wabunge na madiwani hao kutaka
kujiunga na CCM ni kutokana na kukubali kazi inayofanywa na serikali na
kuungwa na wananchi.
Amesema kutokana na kazi kukubalika na wananchi wameona wakiendelea kukaa upinzani 2020 hawatarudi katika nafasi zao.
No comments:
Post a Comment