Chadema wasitisha kampeni ubunge Kinondoni....soma habari kamili na matukio360....#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
CHAMA cha Chadema kimesitisha kampeni ya kumnadi mgombea ubunge wa chama hicho jimbo la Kinondoni jijini Dar es salaam, Salum Mwalimu ili kutoa nafasi kwa wananchi kushiriki katika mazishi ya mwanasiasa mkongwe Kingunge Kongambale Mwiru.
Freeman Mbowe
Kingunge anazikwa leo katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam. Uamuzi was kusitisha kampeni ulitangazwa jana na mwenyekiti taifa wa Chadema, Freeman Mbowe katika mkutano was hadhara uliofanyika katika viwanja vya kwa manyanya Kinondoni.
Mbowe alisema mziba wa Kingunge no mzito kwa kuwa amefanya mengi katika muktaza mzima wa ujenzi wa Tanzania katika uchumi na siasa.
" Katika taifa hili la Tanzania mmoja wa watu waliotumia muda, nguvu na akili kwa ujenzi wa taifa hili ni mzee wetu Kingunge hivyo kesho(leo) tunasitisha kampeni za ubunge ili wananchi washiriki kutoa heshima ya mwisho kwa Mzee Kingunge," alisema Mbowe
Uchaguzi mdogo wa marudio wa jimbo la Kinondoni unatarajiwa kufanyika Februari 17, 2018. Unatanyika kufuatia aliyeikuwa mbunge wa jimbo hilo Kwa tiketi ya chama cha CUF, Maulid Mtulia kujiuzulu na kujiunga CCM. Na sasa anagombea kupitia CCM
CHAMA cha Chadema kimesitisha kampeni ya kumnadi mgombea ubunge wa chama hicho jimbo la Kinondoni jijini Dar es salaam, Salum Mwalimu ili kutoa nafasi kwa wananchi kushiriki katika mazishi ya mwanasiasa mkongwe Kingunge Kongambale Mwiru.
Freeman Mbowe
Kingunge anazikwa leo katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam. Uamuzi was kusitisha kampeni ulitangazwa jana na mwenyekiti taifa wa Chadema, Freeman Mbowe katika mkutano was hadhara uliofanyika katika viwanja vya kwa manyanya Kinondoni.
Mbowe alisema mziba wa Kingunge no mzito kwa kuwa amefanya mengi katika muktaza mzima wa ujenzi wa Tanzania katika uchumi na siasa.
" Katika taifa hili la Tanzania mmoja wa watu waliotumia muda, nguvu na akili kwa ujenzi wa taifa hili ni mzee wetu Kingunge hivyo kesho(leo) tunasitisha kampeni za ubunge ili wananchi washiriki kutoa heshima ya mwisho kwa Mzee Kingunge," alisema Mbowe
Uchaguzi mdogo wa marudio wa jimbo la Kinondoni unatarajiwa kufanyika Februari 17, 2018. Unatanyika kufuatia aliyeikuwa mbunge wa jimbo hilo Kwa tiketi ya chama cha CUF, Maulid Mtulia kujiuzulu na kujiunga CCM. Na sasa anagombea kupitia CCM
No comments:
Post a Comment