LHRC wamkosoa Paul Makonda.... soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimekosoa utendaji wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ikidai  umegubikwa na ukiukwaji utawala wa sheria kwenye utekelezaji wa majukumu yake.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Felista Mauya, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo

Hatua hii ya LHRC inakuja siku chache baada ya mkuu huyo wa mkoa kusimamisha utendaji wa mabaraza ya ardhi ya kata kinyume na sheria pamoja na kudaiwa kuingilia muhimili wa mahakama katika mkutano baina yake na wakazi wa jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kaimu mkurugenzi mtendaji wa LHRC, Felista Mauya amesema kupitia utendaji kazi wa serikali kumekuwepo na juhudi mbali mbali za kuboresha ustawi wa maisha ya wananchi ikiwemo kuwakutanisha wananchi, kuwasikiliza na kuweka mikakati bora ya kutatua kero zao.

“Hata hivyo ombwe la viongozi wa serikali kutofuata taratibu na sheria katika utekelezaji wa majukumu yao limeendelea kuathiri uhalali wa juhudi hizo,” amesema Mauya.

Ameongeza “Kupitia mkutano wa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na wananchi wa Dar es Salaam uliofanyika Februali 10, 2018, LHRC kimebaini mapungufu kadhaa ambayo yamekuwa yakifanywa si tu na Paul Makonda pekee bali pia na baadhi ya viongozi wengine wa serikali baadhi ya mapungufu ya kisheria yanayotokana na mkutano huo ni pamoja na kusimamisha utendaji wa mabaraza ya ardhi ya  kata kinyume na sheria na kuingilia muhimili wa mahakama."

Mauya amewakumbusha viongozi wa serikali na wanasiasa kuwa hawana mamlaka ya kisheria kuingilia utendajikazi wa mahakama wala kuelekeza utendaji wa mahakama badala yake wanapaswa kuheshimu na kufuata taratibu za kimahakama katika upatikanaji wa haki.

Mapendekezo
Amesema kwa kutambua uwepo wa changamoto za kiuwajibikaji miongoni mwa watumishi wa umma na changamoto za kiutendaji wa serikali hasa katika mfumo wa utoaji haki nchini, wametoa mapendekezo saba, miongoni mwa mapendekezo hayo ni..

Serikali kufuata taratibu za kisehria katika kutatua kero na changamoto mbali mbali, watendaji wa serikali hasa katika nafasi za kisiasa wanapaswa kuachakutumia mbinu za kisiasa, badala yake wanapaswa kufuata taratibu zilizopo kisheria ili kutatua changamoto na kero za wananchi kwa maendeleo endelevu.

Viongozi wa kisiasa kuacha kutumia mamlaka yao majukwaani kuwajibisha watumishi wa umma badala yake kufuata taratibu kama zilivyoainishwa katika sheria ya utumishi wa umma ya 2002.

Watendaji wa serikali kuheshimu muhimili wa mahakama, viongozi wa serikali wameapa kulinda katiba kupitia Ibara 107 inaipa mahakama mamlaka  ya juu katika kutenda haki.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search