Mchezaji Juma Nyoso kifungoni tena....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMATI ya nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) imetangaza kumfungia michezo mitano na faini ya sh.milioni 1 beki wa Kagera Sugar Juma Nyoso  kwa kosa la kupiga shabiki baada ya mchezo kati ya timu yake dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba.
Juma Nyoso
Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Ofisa habari wa TFF Clifford Ndimbo, uamuzi huo umefikiwa baada ya shauri lake kufikishwa kwenye kamati hiyo.
“Kamati imemtia hatiani Juma Nyoso kupitia kanuni za ligi kuu na katiba ya TFF lakini ilipokea taarifa za nyuma za Nyoso kwamba aliwahi kuadhibiwa kwa makosa ya utovu wa nidhamu. Kwa hiyo kamati imemfungia Nyoso mechi tano pamoja na faini ya shilingi 1,000,000 (milioni moja),” amesema Ndimbo.
Kwa  mujibu wa Ndimbo  Nyoso alituhumiwa kumpiga shabiki baada ya kumalika kwa mchezo kinyume na kanuni za ligi kuu zinazozungumzia mchezo wa kiungwana.
Hivyo kamati ilipitia ripoti ya kamishna wa mchezo ambayo imeeleza tukio la kupishana kwa Nyoso na shabiki ambaye alikuwa amebeba vuvuzela na mchezaji huyo akaonekana kusimama na kuanza kumpiga shabiki kwa kutumia kiatu na baadaye akamuinamisha na kuanza kumpiga kwa kutumia goti.
Kamati ilimwita Nyoso kujitetea, kwa upande wake alikataa madai hayo ya kumpiga shabiki. Alisema alichofanya ilikuwa ni kumkunja tu shabiki huyo lakini hakumpiga.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search