Maelfu wauaga mwili wa Akwilina....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es salaam

WAZIRI wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako leo ameongoza maelfu ya wakazi wa Dar es salaam kuaga mwili wa marehemu Akwilina Akwilini.

Shughuli hiyo imefanyika katika viwanja vya chuo cha usafirishaji (NIT). Mwili uliwasili majira ya saa sita mchana na ibada ya sala ikiongozwa na kanisa Katoliki ilianza saa saba hadi nane mchana  na ulianza kuagwa saa nane hadi majira ya Alasir.


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiaga mwili wa Akwilina Akwilini

Wasifu wa marehemu:
Alizaliwa Apri 1, 1996 mkaani Kilimanjaro, wilayani Rombo kijiji Olele-Marangu.

Ni mtoto wa sita kati ya watoto nane wa mzee Akwilini Shirima.

Safari yake ya kielimu alianzia katika shule ya msingi kipogolela darasa la kwanza hadi la saba 2007-2014.

Alijiunga na kidato cha kwanza shule ya sekondari High Land iliyoko mkoani Iringa 2011 hadi 2014.

Alijiunga na kidato cha 5 na 6 Embarai Arusha na baadae Lugalo high School mkoani Iringa 2015 hadi 2017.

Hadi anafariki alikuwa akisoma katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) alichojiunga nacho Oktoba 30, 2017 akisomea shahada ya ugavi na usafirishaji na alikuwa mwaka wa kwanza.

Picha zaidi;







About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search