Majaliwa: Mabalozi tafuteni wawekezaji sekta ya utalii...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa
amewataka mabalozi watumieni mbinu za kidiplomasia kuvutia wawekezaji katika
sekta mbalimbali ikiwemo ya utalii na kutafuta masoko ya bidhaa zinazozalishwa
nchini.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ameagana Ofisini kwake Dar es salaam na
Mabalozi wanao kwenda kuiwakilisha Tanzania katika nchi walizo pangiwa,kulia ni
Balozi anaye kwenda Nchini Sweden.Dr Wilbroad Slaa .na kushoto ni Balozi
anayekwenda nchini Nigeria Balozi Muhidin Ally Mboweto
Pia amewataka
mabalozi hao wakaimarishe diplomasia kwa lengo la kuzifanya nchi hizo ziendelee
kushirikiana na Tanzania katika shughuli za kiuchumi na kijamii.
Ametoa kauli hiyo leo
wakati akizungumza na Balozi Dk. Wilbrod
Slaa anayewakilisha Tanzania nchini Sweden na Balozi Muhidin Ally Mboweto
anayewakilisha Tazania nchini Nigeria, katika makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay
jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu amesema
Tanzania ina vivutio vingi vya utalii kama uwepo wa fukwe za bahari kuanzia
Tanga hadi Mtwara, maziwa na mito, mbuga za wanyama hivyo ni vema wakajielekeza
katika kuvutia wawawekezaji kwenye sekta hiyo ili Taifa lipate watalii wengi.
Amesema mbali na
kutangaza sekta ya utalii, pia watafute wawekezaji kwa ajili ya kuwekeza kwenye
sekta ya madini, viwanda na kutafuta masoko ili wafanyabiashara na wakulima wa
Tanzania waweze kuuza bidhaa zao nje ya nchi.
“Tumejiimarisha
katika mazao ya chakula na biashara, hivyo tunatakiwa kuwa na uhakika wa masoko
kwenye kilimo ili mkulima anapozalisha pamba, tumbaku, kahawa, chai, korosho,
dengu pamoja na mazao mengine tuwe na mahali pa kuuza, kwa hiyo washawishini
wafanyabiashara kuja kununua.”
Pia Waziri Mkuu
amewataka mabalozi hao wakawatambue na kuwaunganisha Watanzania waishio kwenye
nchi wanazoiwakilisha ili nao washiriki kwenye ujenzi wa uchumi wa viwanda na
wawasisitize wafuate sheria za nchi wanazoishi na wakumbuke nyumbani.
Waziri Mkuu
amewasisitiza mabalozi hao kwenda kupunguza gharama za uendeshaji wa Balozi kwa
kuzuia matumizi katika mambo yasiyo ya lazima. “Pia maslahi ya nchi lazima
mkayasimamie huko muendako hasa katika masuala ya kiuchumi”
Kwa upande wao
mabalozi hao wamesema watahakikisha wanayafanyia kazi maelekezo yote
waliyopewa ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na nchi
wanazoziwakilisha.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
akisalimiana na Balozi anaye kwenda kuiwakilisha Tanzania katika Nchi ya Sweden
Balozi Dr. Wilbrodi Slaa . kushoto kwa Waziri Mkuu ni Balozi anyekwenda Nchini
Nigeria Balozi Muhidin Ally Mboweto.Mabalozi hao walifika ofisi kwa
Waziri Mkuu Dar es salaam kwa ajili ya kumuaga .
No comments:
Post a Comment