TFF kuendeleza viwanja tisa nchini...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
SHIRIKISHO
la Soka Tanzania (TFF) kuendeleza viwanja tisa nchini kufuatia kuongezeka kwa
dau la pesa za Maendeleo na Kujiendesha zinazotolewa na Shirikisho la Mpira wa
Miguu Duniani FIFA kuanzia mwaka 2019 .
Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk.Harrison
Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu mambo
mbalimbali serikali iliyozungumza na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
Duniani Gianni Infantino na Rais wa CAF Ahmad Ahamad alipokuwa nchini kwa ajili
ya mkutano wao jijini Dar es Salaam
Kauli hiyo imetolewa leo jijini
Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison
Mwakyembe alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kuhusu mambo mbalimbali
serikali iliyojadili na Rais wa FIFA Gianni Infantino alipokuwa nchini kwa
mkutano wake hivi karibuni.
‘’Rais wa FIFA alieleza kuongeza
mara nne ya kiwango cha pesa za maendeleo na kujiendesha walizokuwa wanatoa kwa
mashirikisho kama TFF mpaka kufikia Dola Milioni Moja na Laki Mbili na Nusu kwa
mwaka na kusema pesa hizo ndiyo zitumike kuendeleza viwanja vya michezo kwani
uwepo wa viwanja ndio unaosaidia kukuza vipaji vya soka,’’alisema Dkt.Mwakyembe.
Akiendelea kuzungumza katika
mkutano huo na waandishi wa habari Waziri Mwakyembe alisisitiza kuwa Rais huyo
wa FIFA ametoa msisitizo wa kutokuwa na huruma kwa kiongozi yoyote wa
shirikisho atakayekuwa na matumizi mabaya ya pesa pamoja na kufanya udanganyifu
kwani yeye yuko mstari wa mbele kupinga ufisadi katika sekta ya maendeleo ya
Soka duniani.
Pamoja na hayo nae Rais wa TFF
Bw. Wallace Karia alitoa ufafanuzi wa hali ya kifedha kwa shirikisho na
kueleza kufuatia kuwepo na matatizo katika shirikisho hilo FIFA ilikuwa
imesitisha kuwapatia fedha hizo za maendeleo na kujiendesha tangu mwaka 2015
lakini baada ya kuingia uongozi mpya ambao FIFA wameridhika nao na wameshaupa
utaratibu wa kufuatilia fedha hizo.
‘’Rais wa FIFA alitueleza kuwa
fedha hizo ziko salama nchini Zurich ni kwamba tu hazikuwa zimeruhusiwa kuingia
nchini na kwa sasa tumeshaanza mchakato wa kufuatilia fedha hizo kwa kuzingatia
maelekezo ya FIFA hivyo basi tutakapo pata fedha hizo Shirikisho
litaendeleza baadhi ya miradi ambayo tumekwisha iandaa,’’alisema Bw.
Karia.
Pamoja na hayo rais huyo alitoa
wito wa wakazi wa jiji la Tanga waliyovamia eneo linalotarajia kujengwa
Technical Center ya mchezo wa soka basi waondoke mara moja kabla
hawajachukuliwa hatua.
No comments:
Post a Comment