MAJALIWA: Watendaji, wakuu wa idara nendeni vijijini...soma habari kamili na matukio360...#share
Na
Mwandishi Wetu, Mwanza
WAZIRI
Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watendaji na wakuu wa idara mbalimbali
kuhakikisha wanatenga muda na kwenda vijijini kuwahudumia wananchi.
Amesema wananchi hususani waishio maeneo ya vijijini wanachangamoto mbalimbali ambazo zinatakiwa kupatiwa ufumbuzi na watendaji hao.
Amesema wananchi hususani waishio maeneo ya vijijini wanachangamoto mbalimbali ambazo zinatakiwa kupatiwa ufumbuzi na watendaji hao.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa mmiliki wa kiwanda kidogo cha Dotto Posho Mill, Alexander Dotto (kushoto) kuhusu unga na Mchele unaozalishwa na kiwanda hicho kilichopo eneo la Bukara, Sengerema Februari 15, 2018. Kulia ni mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Waziri Mkuu, aliyasema hayo jana (Alhamisi,
Februari 15, 2018) alipozungumza kwa nyakati tofauti na watumishi na wananchi
katika kata ya Nyehunge na Ibisabageni wilayani Sengerema akiwa katika ziara ya
mkoa wa Mwanza.
Alisema
Serikali imedhamiria kwa dhati kuwatumikia kwa lengo la kuwaondolea kero
mbalimbali zinazowakabili, hivyo hakuna sababu ya watendaji kukaa maofisini.“Watumishi wanawajibu
wa kuwafuata wananchi katika maeneo yao hasa vijijini kwa sababu si kila
mwananchi anauwezo wa kufuata huduma katika ofisi zenu na atakayeshindwa
kufanya hivyo hatutomvumilia.”
Waziri
Mkuu aliongeza kuwa Serikali inawawezesha watumishi wake kwa kuwapatia vitendea
kazi kama usafiri ili waweze kuwahudumia wananchi ipasavyo.Alisema kwa sababu ya
kutotekeleza wajibu wao ipasavyo kumekuwa na kero na malalamiko mengi kutoka
kwa wananchi na hivyo kusababisha wananchi kuwasilisha kero na malalamiko hayo
wakati wa ziara za viongozi wakuu.
Katika
hatua nyingine Waziri Mkuu aliwataka wananchi wanaofanya kazi katika kiwanda
cha kuongeza thamani ya mazao ya nafaka cha Doto Alex Posho Meel kuwa waaminifu.Waziri Mkuu alisema
wafanyakazi hao wanatakiwa wawe waaminifu na
wafanye kazi kwa bidii ili kukiwezesha kiwanda hicho kuendelea na uzalishaji.
No comments:
Post a Comment