Mbowe, wenzake wahojiwa kwa saa nne, waachiwa kwa dhamana...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es salaam

VIONGOZI wakuu sita wa Chadema akiwamo Freeman Mbowe wamehojiwa kwa saa nne katika kituo cha polisi kati jijini Dar es salaam, taarifa zinadai mahojiano yalihusu kufanya maandamano Februari 16,2018 bila kuwa na kibali.

Wengine ni John Mnyika, Halima Mdee, John Mrema, Salum Mwalimu, Ester Matiko na John Heche. Wamehojiwa  kuanzia saa saa nane mchana hadi saa 12 Alasir

Freeman Mbowe

Hata hivyo wote wameachiwa kwa dhamana huku Mbowe akiondoka kwa eskoti ya polisi na watarejea hapo Machi 5,2018


Hatua hiyo inafuatia wiki iliyopita baadhi ya viongozi hao kufika kituoani hapo na kutakiwa kurejea leo majira ya saa nne asubuhi kuitikia wito wa kamanda jeshi la polisi Dar es salaam, Lazaro Mambosasa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search