TANNA walaani muuguzi kupigwa....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu

Chama Cha Wauguzi Nchini (TANNA) kimelaani tukio la shambulio la muuguzi lililotokea Februari 18, 2018 katika Hosptali ya Bugando jijini Mwanza na ndugu wa mgonjwa ambaye muuguzi huyo alikuwa akimuhudumia na kufariki dunia.

Makamu wa rais wa TANNA Dk. Ibrahim Mgoo, amesema  kabla ya shambulio hilo muuguzi alitimiza wajibu wake wa kazi , alishambuliwa na watu wanaojulikana waliokuwa na kusudi la kutoa uhai katika chumba cha uangalizi maalumu (HDU), Hospitalini hapo, ambapo ni kinyume na taratibu za hosptali hiyo.

“Kabla ya mauti kumfika mgonjwa huyo ndugu zake walilazimisha wabaki katika chumba hicho jambo ambalo, halikukubaliwa na muuguzi huyo, kesho yake walipotaarifiwa ndugu yao amefariki, ndipo walipoamua kufanya kitendo cha unyama na udhalilishaji kwa kumshambulia na kumjeruhi muuguzi alipokuwa anatoa huduma kwa wagonjwa wengine”, alisema.

Makamu Mgoo, ameviomba vyombo vinavyohusika kuchukua hatua stahiki, kwa wahusika mapema ili kutoathiri utendaji wa wauguzi nchini, ikiwa ni pamoja na kuboresha ulinzi wa wauguzi na watumishi wengine mahala pa kazi ili kutoleta madhara makubwa katika kazi.

Aidha, ametoa shukrani kwa hatua zilizochukuliwa na uongozi wa Hospitali ya Bugando ukishirikiana na chama cha wauguzi, kuhakikisha Muuguzi huyo anatendewa haki katika vyombo vinavyohusika.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search