Mwanasiasa Tambwe Hizza kuzikwa leo....soma habari kamili na matukio360....#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
MWANASIASA wa siku nyingi, Tambwe Hizza aliyefariki jana alfajiri atazikwa leo
jijini Dar es salaam katika makaburi ya Chang'ombe wilayani Temeke.
jijini Dar es salaam katika makaburi ya Chang'ombe wilayani Temeke.
Tambwe Hizza
Mmoja wa wanafamilia, Charles Hizza ameiambia matukio360 kuwa Hizza alifariki njiani akiwa ndani ya gari lake alipokuwa akielekea hospitali kupata matibabu ya ugonjwa wa pumu.
Amesema baada ya kuzidiwa mmoja wa wasamalia wema alimuona na kuingia garini na kumkimbiza hospitali.
Ndugu huyo amesema kabla ya umauti, usiku alisumbuliwa na tatizo Hilo na kulipopambazuka alilazimika kwenda haraka hospitali iliyopo Mbagala Kizuiani.
"Lakini hakufika, alifariki njiani akiwa katika gari lake. Ratiba zikikamilika mapema atazikwa leo(Ijumaa) Alasiri katika makaburi ya Chang'ombe Temeke," amesema
Tambwe aliyezaliwa mwaka 1959, ameacha mjane na watoto watatu na mmoja wa waratibu wa kampeni za chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika jimbo la Kinondoni akiwa ni meneja kampeni msaidizi wa mgombea ubunge, Salum Mwalimu.
Kabla ya kuipigia debe Chadema, Hizza alikuwa ni kiongozi mwandamizi wa chama cha CUF baadae iling'atuka na kujiunga CCM.
Umaarufu wake uliongezeka mwaka 2005 na 2010 alipogombea ubunge katika jimbo la Temeke jijini Dar es salaam kwa tiketi ya CUF
Umaarufu wake uliongezeka mwaka 2005 na 2010 alipogombea ubunge katika jimbo la Temeke jijini Dar es salaam kwa tiketi ya CUF
Kwa mara ya kwanza aliibuka na kuipigia debe Chadema kwa mwamvuli wa Ukawa kwenye ufunguzi wa kampeni wa uchaguzi mkuu mwaka 2015.
No comments:
Post a Comment