Samia Suluhu atoa pole kifo rubani wa ndege za serikali....soma habari kamili na matukio360....#share
Makamu wa rais Samia Suluhu Hassan leo amehudhuria msiba wa
Rubani wa Ndege za Serikali, Marehemu Kapteni Dominic Bomani aliyefariki jana
kwa ajali ya ndege kwenye uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume.
Makamu wa rais Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha
kumbukumbu cha maombelezo ya Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni
Dominic Bomani nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani.
Makamu wa rais Samia Suluhu Hassan akimpa pole Rosemary
Bomani mjane wa aliyekuwa Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic
Bomani nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani.
Makamu wa rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rosemary
Bomani mjane wa aliyekuwa Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic
Bomani, wengine pichani ni mtoto wa marehemu Joanitha Bomani (kulia) na Dada wa
marehemu Stella Bomani(kushoto) wakati alipoenda kuwapa pole nyumbani kwa
marehemu Kinyerezi Kanisani.
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
No comments:
Post a Comment