Sugu, Masonga waachiwa kwa dhamana....soma habari kamili na matukio360...#share


Na mwandishi wetu, Mbeya

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi "Jongwe" pamoja na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga wameachiwa kwa dhamana.

Wanakabiliwa na kesi  ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli. 



Sugu na Masonga wamekaa mahabusu kwa muda wa siku 24 baada ya kunyimwa dhamana na mahakama hiyo kutokana na...

hoja za upande wa  Jamhuri. 

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya hakimu mkazi Mbeya, Michael Mteite leo amewaachia kwa dhamana  baada ya Wakili upande wa utetezi, Peter Kibatala kuiambia mahakama hiyo kwamba imeshafunga ushahidi wake ambapo mashahidi sita walitoa ushahidi wao.
 

Mawakili wa pande zote mbili walikubaliana kwamba Februari 19 watawasilisha majumuisho ya shauri hilo mahakamani hapo.
 

Hakimu Mteite amekubaliana  na hoja hiyo ya mawakili na kusema hukumu ya kesi hiyo itatolewa Februari26 mwaka huu.
 

"Washtakiwa wote wanaachiwa kwa dhamana, na kila mmoja atajidhamini mwenyewe kwa hati ya dhamana ya maneno ya Sh5 milioni kwa kila mmoja.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search