TGNP waandaa kongamano la wanawake na uongozi...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Karoli Vinsent, Dar es Salaam

MTANDAO  wa Jinsia (TGNP) wameandaa kongamano la Wanawake na Uongozi kwa ajili ya kutoa fursa  kwa wanawake waweze kujitafakari na kujitathimini.
Pichani ni Mkurugenzi mtendaji wa (TGNP) Lilian Liundi akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaamm, Mkurugenzi mtendaji wa (TGNP) Lilian Liundi  amesema Kongamano hilo litatoa fursa kwa wanawake na wadau  wengine kujitafakari ,kutathimini,kusherekea na kupanga mikakati ya kuimarisha ushiriki wa wanawake katika uongozi.

Amesema Kongamano hilo litawakutanisha wanawake Viongozi na wadau wengine wa masuala ya usawa wa kijinsia.

"Tutakuwa  na michango ya wanawake katika nyanja mbali mbali za maendeleo,kushirikishana uzoefu,changamoto na kutoa mapendekezo ya namna ya kukabiliana nazo changamoto zinazowakabili wanawake"Amesema Liundi.

Amesema Kongamano hilo la litafanyika siku ya jumanne tarehe 27 Februari 2018  katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam na  katika Kongamano hilo linatarajiwa  kukutanisha washiriki 250 wakiwemo baadhi ya viongozi.
"Katika Kongamano hili kutakuwepo na viongozi wanasiasa wastaafu,viongozi wanawake na wanaume walioko madarakani hivi sasa, wabunge na madiwani,pamoja asasi za kiraia ,wawakilishi kutoka serikalini"Ameongeza kusema .

Hata Hivyo, Liundi amesema katika kongamano hilo kutakuwa na fursa ya kipekee ya kutafakari kuhusu kazi zisizo kuwa na kipato ikiwemo Kulea familia ,wazazi ,wagonjwa ,watu wanaoishi na Ulemavu. 

"TGNP  mtandao  tumetoa wito kwa serikali kuanza kutambua na kuthaminisha kazi hizi ili iweze kuingia katika Pato la Taifa,kazi hizi zinamchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Taifa"amesema 


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search