Watano wafariki, sita wajeruhiwa katika ajali...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Tanga
WATU watano wamefariki papo hapo na wengine sita kujeruhiwa katika ajali iliyotokea jana katika barabara ya Segera- Kabuku wilayani Hadeni mkoani Tanga.
SIMANZI: Hivi ndivyo ajali ya Basi la AJ_Safari ilovyotokea ,Baada ya basi hilo kugongana uso kwa uso na gari dogo aina ya Hiace katika kijiji cha Kabuku Wilayani Handeni Mkoani Tanga.
Kaimu kamanda mkoa wa Tanga Leon Rwegasira ameiambia matukio360 kuwa ajali hiyo imehusisha magari mawili, Hiace na basi kubwa aina ya Youtong.
Amesema dereva wa hiace ni miongoni mwa waliofariki na kwamba wanamshikiria dereva wa basi ambaye ni mkazi wa Dar es salaam.
"Hadi sasa bado hatujajua chanzo cha ajali, tulichofanya ni kuokoa majeruhi na hali zao zikitengemaa tutawauliza majina yao, wanapoishi na sababu za ajali. Lakini hadi ninavyoongea watano wamefariki na sita wamejeruhiwa," amesema Rwegasira
Amesema basi hilo lilikuwa linatoka Tanga kwenda Dar es salaam
WATU watano wamefariki papo hapo na wengine sita kujeruhiwa katika ajali iliyotokea jana katika barabara ya Segera- Kabuku wilayani Hadeni mkoani Tanga.
SIMANZI: Hivi ndivyo ajali ya Basi la AJ_Safari ilovyotokea ,Baada ya basi hilo kugongana uso kwa uso na gari dogo aina ya Hiace katika kijiji cha Kabuku Wilayani Handeni Mkoani Tanga.
Amesema dereva wa hiace ni miongoni mwa waliofariki na kwamba wanamshikiria dereva wa basi ambaye ni mkazi wa Dar es salaam.
"Hadi sasa bado hatujajua chanzo cha ajali, tulichofanya ni kuokoa majeruhi na hali zao zikitengemaa tutawauliza majina yao, wanapoishi na sababu za ajali. Lakini hadi ninavyoongea watano wamefariki na sita wamejeruhiwa," amesema Rwegasira
Amesema basi hilo lilikuwa linatoka Tanga kwenda Dar es salaam
No comments:
Post a Comment