Waziri Mwigulu awaonya askari magereza....soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Geita
WAZIRI wa Mambo ya ndani ya nchi, Dk Mwigulu Nchemba amewataka askari wa jeshi la magereza kufanya kazi kwa weledi na kufata maadili ya kazi.
Waziri Nchemba akifungua gereza wilayani Chato mkoani Geita
Waziri Dk Mwigulu meyasema hayo akifungua gereza la wilaya ya Chato mkoa wa Geita jana.
Amesema kuna taarifa ya baadhi ya askari wanaokiuka maadili ya kazi na masharti ya wahalifu wawapo magerezani kwa kushirikiana nao kwa kuwapa simu na vitu vingine ambavyo ni kinyume cha sheria na maadili ya kazi yao.
Amesema sasa majira yamebadilika na aina ya wahalifu wamebadilika ni wajibu wa askari kuzingatia maadili ya kazi kuliko walivyokuwa wakifanya zamani enzi watanzania wote wakiwa ndugu na wahalifu.
"Kuna taarifa za rejareja za baadhi ya magereza vijana wetu wanawapa simu wafungwa kuwasiliana na jamaa zao, zamani unaweza fikilia anasalimia familia lakini si sasa unaweza mpa simu kumbe anapanga mpango wa kuwateka, majira yamebadilika. Sheria zipo basi tuzingatie sheria na maadili ya kazi zetu".alisema Dk Mwigulu.
Waziri huyo amesema magereza yajengwa ili kusaidia wanaopata matatizo lakini serikali inataka watu wasifanye makosa kupelekwa magerezani.
Mkuu wa jeshi la magereza, kamishna jenerali wa magereza Dk. Juma Malewa amesema changamoto kubwa wanazokabiliana nazo baada ya kufungua gereza ni usafiri, upungufu wa askari na wanapofungua gereza jipya huitaji askari wasiopungua 50 na changamoto nyingine ni miundombinu chakavu ya magereza
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Geita, Eng. Gabriel Robert amesema mkoa umejipanga kuhakikisha wanatoa ardhi kwa jeshi la magereza kwa ajili ya kilimo na ufugaji ili lijitegemee
katika chakula na kiuchumi
WAZIRI wa Mambo ya ndani ya nchi, Dk Mwigulu Nchemba amewataka askari wa jeshi la magereza kufanya kazi kwa weledi na kufata maadili ya kazi.
Waziri Nchemba akifungua gereza wilayani Chato mkoani Geita
Waziri Dk Mwigulu meyasema hayo akifungua gereza la wilaya ya Chato mkoa wa Geita jana.
Amesema kuna taarifa ya baadhi ya askari wanaokiuka maadili ya kazi na masharti ya wahalifu wawapo magerezani kwa kushirikiana nao kwa kuwapa simu na vitu vingine ambavyo ni kinyume cha sheria na maadili ya kazi yao.
Amesema sasa majira yamebadilika na aina ya wahalifu wamebadilika ni wajibu wa askari kuzingatia maadili ya kazi kuliko walivyokuwa wakifanya zamani enzi watanzania wote wakiwa ndugu na wahalifu.
"Kuna taarifa za rejareja za baadhi ya magereza vijana wetu wanawapa simu wafungwa kuwasiliana na jamaa zao, zamani unaweza fikilia anasalimia familia lakini si sasa unaweza mpa simu kumbe anapanga mpango wa kuwateka, majira yamebadilika. Sheria zipo basi tuzingatie sheria na maadili ya kazi zetu".alisema Dk Mwigulu.
Waziri huyo amesema magereza yajengwa ili kusaidia wanaopata matatizo lakini serikali inataka watu wasifanye makosa kupelekwa magerezani.
Mkuu wa jeshi la magereza, kamishna jenerali wa magereza Dk. Juma Malewa amesema changamoto kubwa wanazokabiliana nazo baada ya kufungua gereza ni usafiri, upungufu wa askari na wanapofungua gereza jipya huitaji askari wasiopungua 50 na changamoto nyingine ni miundombinu chakavu ya magereza
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Geita, Eng. Gabriel Robert amesema mkoa umejipanga kuhakikisha wanatoa ardhi kwa jeshi la magereza kwa ajili ya kilimo na ufugaji ili lijitegemee
katika chakula na kiuchumi




No comments:
Post a Comment