Mke Tsvangirai kutohudhulia maziko ya mume wake....soma habari kamili na matukio360....#share
Na mashirika ya kimataifa
WAKATI leo mchana kiongozi wa chama cha MDC, Morgan Tsvangirai atazikwa kijijini kwao Buhera, mke wake Elizabeth Macheka, hatokuwepo.
Hatua hiyo inatokana na kupoteza fahamu kutokana na presha kupanda na familia kulazimika kumuacha mjini Harare na kuzuia asishiriki maziko hayo
WAKATI leo mchana kiongozi wa chama cha MDC, Morgan Tsvangirai atazikwa kijijini kwao Buhera, mke wake Elizabeth Macheka, hatokuwepo.
Hatua hiyo inatokana na kupoteza fahamu kutokana na presha kupanda na familia kulazimika kumuacha mjini Harare na kuzuia asishiriki maziko hayo
Jeneza lenye mwili wa Morgan Tsvangirai
Jana majira ya mchana mamia ya Wazimbabwe walitoa heshima za mwisho kwa kuuaga mwili wa kiongozi huyo katika viwanja vya shule ya msingi Makanda.
Mwili wa Tsvangirai uliwasili hapo kwa helkopta mbili za jeshi la Zimbabwe, ukishindikizwa na mama mzazi wa kiongozi huyo, Mbuya Lydia Chibwe Tsvangirai, kaka yake Collin na mtoto wake Edwin.
Mwili wa Tsvangirai uliwasili hapo kwa helkopta mbili za jeshi la Zimbabwe, ukishindikizwa na mama mzazi wa kiongozi huyo, Mbuya Lydia Chibwe Tsvangirai, kaka yake Collin na mtoto wake Edwin.
Makamo mwenyekiti wa MDC, Messrs Nelson Chamisa na Elias Mudzuri ambaye anatarajiwa kuongoza chama hicho hawakupanda helkopta hizo.
Mama wa Morgan alilazimika kumzuia Elizabeth asihudhulie maziko, akihofia anaweza kupoteza maisha.
Morgan Tsvangirai alifariki hivi karibuni nchini Afrika Kusini kwa ugonjwa wa kansa ya utumbo.
Miongoni mwa viongozi watakaohudhulia maziko hayo ni rais wa Zimbabwe, Emerson Mnagangwa na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga.
Mama wa Morgan alilazimika kumzuia Elizabeth asihudhulie maziko, akihofia anaweza kupoteza maisha.
Morgan Tsvangirai alifariki hivi karibuni nchini Afrika Kusini kwa ugonjwa wa kansa ya utumbo.
Miongoni mwa viongozi watakaohudhulia maziko hayo ni rais wa Zimbabwe, Emerson Mnagangwa na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga.




No comments:
Post a Comment