Jinsi polisi Dodoma walivyowakamata wahamasishaji maandamano....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dodoma


JESHI la polisi mkoa wa Dodoma linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuhamasisha maandamano kwenye mitandao ya kijamii yanayotarajiwa kufanyika April 26 mwaka huu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto akiwa amewatazama watuhumiwa wa uhamasishaji wa maandamano.

Kamanda wa polisi wa mkoa Dodoma Gilles Muroto akizumgumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma, amesema watu hao wamekua wakisambaza ujumbe kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu kuandamana huku wakijua ni kosa kisheria.

Kamanda Mruto ametoa wito kwa watu kutofuata mkumbo kuhamasisha watu kufanya maandamano kwani ni kosa kisheria na kuwa yeyote ambaye atakamatwa atashughulikiwa kisheria.

"Watu hawa wamekuwa wakihamasisha wananchi kufanya maandamano, tulishasema Serikali haijalibiwi leo tunaanza kutoa mifano kwao. Wale wote wanaoijaribu Serikali tutahakikisha tunawachukulia hatua za hali ya juu sana” amesema

Mbali na hilo Kamanda Mruto amesema kuwa upelelezi ukikamilika watu hao watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao kuhusu kuhamasisha watu kufanya maandamano kupitia mitandao ya kijamii ambayo yamepangwa kufanyika April 26, 2018 nchi nzima na yakiratibiwa na mwanadada Mange Kimambi kupitia mitandao ya kijamii.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search