LHRC waijibu NEC....soma habari kamili na matukio360....#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimejibu hoja za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufuatia kuhusika kutoa tamko lenye tuhuma za kupotosha baadhi ya mambo kupitia tamko la umoja wa asasi za kiraia nchini (Azaki).
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji LHRC, Naemy Sillayo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Hivi karibuni NEC kupitia kwa mkurugenzi wa uchaguzi  Kailima Ramadhani ilikiandikia barua yenye Kumbukumbu. Na. Bi. 71/75/01/124 ya Februari 22, 2018 ikikituhumu moja kwa moja kuhusika katika upotoshwaji kwenye tamko la juu ya taarifa ya hali ya usalama wa raia, haki za binadamu na utawala bora.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Naemy Sillayo amesema kituo hicho kirishiriki kama moja ya asasi zinazounda umoja wa Azaki.

“Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kama moja ya asasi zinazounda umoja wa Azaki hizo kimelezimika kujibu hoja hizo kwani NEC katika tamko lake lililotolewa Ijumaa Februari 23, 2018 imekituhumu moja kwa moja LHRC kupitia kwa aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi, Bw. Paul Mikongoti, kwa kutoa tamko lenye tuhuma za kupotosha baadhi ya mambo kupitia tamko la hilo la umoja wa Azaki,” amesema Sillayo.

“Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, kilishiriki kwenye tamko hilo kama mwanachama wa Azaki kwa kutambua wazi kuwa lengo la tamko hilo ni kuimarisha hali ya haki za binadamu na demokrasia nchini na si vinginevyo,” ameongeza.

Ameitoa wasiwasi NEC kuwa hakukuwa na maslahi tofauti wala upotoshaji wa makusudi katika utoaji wa tamko hilo.

Amesema kwamba kituo kinakiri kufahamu kwa kina sheria na kanuni zinazoratibu chaguzi na kinatambua kuwa lengo la Azaki haikuwa kubeza wala kuvunja kanuni hizo bali kutoa mapendekezo kwa ajili ya mboresho ya chaguzi na hatimaye kuimarisha demokrasia nchini.

Sillayo ameikumbusha NEC kuwa tamko husika halikutolewa na LHRC bali lilitolewa na umoja wa Azaki chini ya jukwaa la wakurugenzi wa Azaki hivyo haikuwa busara kuwashambulia wao moja kwa moja.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search