MSD yaelezea upatikanaji dawa nchini....soma habari kamili na matukio360....#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
BOHARI ya Dawa nchini
(MSD) imesema upatikanaji dawa muhimu zaidi (high priority list)
ambazo ni 135 umefikia asilimia 90.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Saal.
Hayo yamesemwa na
Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Banakunu alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari leo jijini Dar es Salaam.
“Dawa tunazo nyingi,
hali ya upatikanaji wa dawa imeimarika, kwa mfano leo Machi 7, 2018
upatikanaji wa dawa muhimu zaidi (High priority list) ambazo ni jumla ya 135
umefikia asilimia 90 ukijumlisha na zile zilizopo kwenye maduka ya MSD,”
amesema Bwanakunu.
Amesema dawa
hizo zote zinahitajika katika vituo vyote vya serikali vya kutolea huduma za
afya nchini.
Pia amesema upatikanaji wa dawa hizo muhimu zaidi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ni kati ya asilimia 85 hadi 95, upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI na za kutibu malaria ni asilimia 100.
Pia amesema upatikanaji wa dawa hizo muhimu zaidi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ni kati ya asilimia 85 hadi 95, upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI na za kutibu malaria ni asilimia 100.
Wakati huo huo
upatikanaji dawa za uzazi wa mpango ni asilimia 67 huku za kutibu kifua
kikuu pamoja na ukoma ni asilimia 63.
Katika hatua nyingine
MSD imesema imeanza kutoa huduma ya mifuko yenye vifaa vya kujifungulia
kwa akina mama (Delivery Pack).
Bwanakunu amesema vifaa hivyo vitakuwa vikipatikana kwa bei
nafuu na mfuko huo utakuwa na vifaa 12 na utauzwa kwa sh. 21,000.
Ametaja vifaa hivyo
kuwa ni pamba kubwa (Cotton wool gm.500), mpira wa kuzuia uchafu (Macknitosh
1.5 mters), taulo ya kike ya wazazi (maternity pad) sindano ya kuzuia damu
kupotea (Oxytocin injection) na mipira ya mikono (Surgical gloves 4 pairs).
Vingine
ni nyembe za kupasulia (Surgical blade), kibana kitovu cha mtoto (Umbilical
Cord clamp), dawa ya spirit, detol ya maji, dawa ya sindano ya ganzi
(Lignocaine) mabomba ya sindano mawili na nyuzi za kushonea (Surgical Sutures).
Awali mkurugenzi huyo
amesema MSD imeendelea kukidhi viwango vya ubora vya kimataifa katika
mfumo wa ununuzi, utunzaji na usambazaji dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya
maabara (Supply Chain Management) na kupata ithibati ya kimataifa ya Ubora ya
daraja la juu inayojulikana kama ISO 9001:2015 ambayo itadumu kwa miaka mitatu
(2017-2020).
Jack Reacher Never Go Back is sequel to Tom Cruise movie named Jack Reacher. Second part is directed by Edward Zwick and producer are Tom Cruise,... USA delivery Soma
ReplyDelete