Lipumba afichua siri mgogoro wa CUF...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam
Profesa Ibrahim Lipumba amesema mgogoro unaoendelea ndani ya chama cha CUF ulianzishwa na Maalim Seif Sharif akiwa na lengo la kudhoofisha chama hicho na kuwakumbatia viongozi wa Chadema
Pai amemtuhumu katibu mkuu Maalim Seif Sharif kwa kudhoofisha chama hicho kwa maslahi yake binafsi ya kung'ang’ania kuwa rais wa Zanzibar.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Tuhuma hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa CUF taifa Profesa
Lipumba alipokuwa akizungumza na waandisi wa habari leo jijini Dar es Salaam
juu ya maazimio ya kikao cha baraza kuu la uongozi la taifa kilichofanyika
jijini humo kuanzia Machi 17 hadi 18, 2018.
" Mgogoro unaoendelea ndani ya chama ulianzishwa na Maalim Seif kwa lengo la kudhoofisha chama na kuwakumbatia viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)," amesema Lipumba na kuongeza.
"Pia amekidhoofisha chama kwa maslahi yake binafsi ya kung'ang’ania kuwa rais wa Zanzibar."
" Mgogoro unaoendelea ndani ya chama ulianzishwa na Maalim Seif kwa lengo la kudhoofisha chama na kuwakumbatia viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)," amesema Lipumba na kuongeza.
"Pia amekidhoofisha chama kwa maslahi yake binafsi ya kung'ang’ania kuwa rais wa Zanzibar."
Akizungumzia kuhusu hali ya kisiasa ndani ya chama na nchi
Prof. Lipumba amesema “Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad amekidhoofisha
chama chetu, kwa kutotekeleza azimio la baraza kuu la kufungua kesi mahakama
kuu ya Zanzibar kupinga kufutwa matokeo ya uchaguzi wa wakilishi na madiwani
ambao walikabidhiwa hati za ushindi wa majimbo na shehia zao baada ya uchaguzi
mkuu wa Oktoba 25, 2015,”
Prof. Lipumba ameseama kama kesi hizo zingefunguliwa CUF
ingekuwa na wawakilishi 27 wa majimbo na nusu ya wawakilishi wote wa viti
maalum, pia idadi ya wawakilishi wa kuchaguliwa na wa viti maalum wa CUF
ingekuwa sawa na idadi ya wawakilishi wa CCM.
Ameongeza kwamba kwa kufunguliwa kwa kesi hizo kungefanya kuundwa
kwa serikali ya umoja wa kitaifa ya Zanzibar ingekuwa na mawaziri wa CUF
ambapo kwa hivi sasa wamewaacha chama cha mapinduzi (CCM) peke yao ambao
wanatunga sheria watakavyo wao.
Amesema pamoja na mazingira magumu waliyonayo baraza kuu
limeagiza juhudi kubwa zifanyike kulinda katiba ya Zanzibar ya 2010 inayotaka
kuwepo kwa serikali ya umoja wa kitaifa.
Pia baraza limemshauri Rais John Magufuli kwa nafasi yake
kujiwekea ajenda ya kuimarisha demokrasia nchini ikiwa ni pamoja na kulinda
haki za binadamu, kuheshimu haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara
katika hali ya amani na utulivu na uhuru wa vyombo vya habari kufanya kazi zao
kwa mujibu wa sheria.
Kuhusu hali ya uchumi
nchini
Mwenyekiti huyo wa CUF pamoja na kuipongeza serikali kwa
juhudi zake za kukusanya mapato na kutekeleza miradi mikubwa mbalimbali ya
maendeleo amesema baraza limeitaka iwe na bajeti inayotekelezeka.
Kuhusu chaguzi ndogo za
marudio za serikali
Prof. Lipumba amesema baraza limesikitishwa na kuvunjwa kwa
taratibu katika chaguzi hizo na kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC)
kujirekebisha. Amesema pamoja na mapungufu makubwa katika usimamizi wa uchaguzi
chama kitaendelea kushiriki katika chaguzi hizo.
No comments:
Post a Comment