Maalim Seif auzungumzia waraka wa maaskofu KKKT.... soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif ameunga mkono waraka uliotolewa mwishoni mwa juma na Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili na Kilutheri Tanzania (KKKT) na kutaka wasihusishwe na masuala ya kisiasa.
Katibu Mkuu wa Chama cha CUF Maalim Seif, akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.

Ametoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam alipitakiwa kutoa maoni yake juu ya waraka huo wakati wa maswali baada ya kuwasilisha mbele ya waandishi wa habari maazimio ya kikao cha kamati ya utendaji ya chama cha CUF Taifa kilichofanyika Machi 25, 2018.

“Mimi kama mimi nimefarijika ninaunga mkono kuona viongozi wa dini wanakemea mambo ambayo hayaendi vizuri  na tusitafsiri kuwa wamejiingiza kwenye siasa, kwa kuwa ni viongozi wa kiroho wanawajibu wa kuwatetea waumini wao, ningefarijika sana kama na viongozi wangu wangefanya hivyo,” amesema Maalim.

Katika waraka huo uliopewa jina la ‘Taifa Letu Amani Yetu’ na kusainiwa na Maaskofu 27 wa kanisa hilo uliainisha changamoto mbali mbali zinazolikabili taifa kwenye nyanja za hali ya kiuchumi, maisha ya siasa na masuala mtambuka likiwemo suala la Katiba Mpya.

Katibu Mkuu huyo amesema kuwa lengo la Maaskofu hao siyo kuikosoa serikali bali ni katika hali ya kutaka mambo yaende sawa ambapo ameeleza kufarijika kwa kuona taasisi mbalimbali zikitoa matamko pale zinapoona mambo hayaendi kama inavyotakiwa.

Amewataka watanzani na taasisi mbalimbali nchini kuendelea kupaza sauti na kuikumbusha serikali kuwa jukumu lake la msingi ni kulinda usalama wa raia na mali zao.

Katika hatua nyingine Maalim Seif ametuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya watu 26 waliofariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea juzi Mkuranga Mkoani Pwani.
Ajali hiyo ilihusisha  gari  ndogo ya abiria aina ya Toyota Hiace yenye namba za usajili T.676 DGK inayofanya safari zake Kimanzichana – Mbagala Rangi tatu na gari nyingine aina ya Lori.


 


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search