Atiwa mbaroni kwa kupora, kubaka na kuwapiga wanawake picha za utupu...soma habari kamili na matukio360..#share
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Mabula Mabula maarufu Six mkazi wa mjini humo, kwa tuhuma za uporaji wa simu kwa kutumia
pikipiki, kubaka na kuwapiga picha za utupu wanawake kisha kuzisambaza
mitandaoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei
Akizungumza leo, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ulrich Matei
amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa baada ya makachero, kikosi cha kupambana na
uhalifu mitandaoni pamoja na kikosi cha kupambana na ujambazi,
kumfuatilia kwa ukaribu.
Akihojiwa mara baada ya kukamatwa, Mabula ameeleza mbinu
anazotumia ikiwa ni pamoja na kujifanya askari polisi, kuwakamata wanawake
nyakati za usiku, kuwasingizia makosa mbalimbali na kuwapeleka maeneo yenye
giza na kuwabaka.
Mtuhumiwa huyo ameyataja maeneo anayofanyia matendo hayo kuwa ni
Msamvu Relini na kwamba amekuwa akitumia mapanga kuwatisha wanawake hao na
kuwapiga picha za utupu na baadaye kutishia picha hizo kuzituma kwenye mitandao
ya kijamii.
“Hizo picha huwa nawapiga kwa kutumia simu zao na anayekataa
kunipa hela huwa naondoka na simu yake na kisha natuma hizo picha kwenye
mitandao iliyopo kwenye simu hizo, baada ya hapo simu naiuza napata hela,”
amesema mtuhumiwa huyo.
Katika mahojiano na polisi, mtuhumiwa huyo amemtaja
mwezake mmoja Ramadhani Salumu maarufu Miondoko mkazi wa Manispaa ya Morogoro
kuwa ndio mnunuzi wa simu hizo za wizi.
Katika msako huo polisi wamefanikiwa kumkamata Salumu na kwamba
wote watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
No comments:
Post a Comment